Zaburi 104:1-35

  • Kumsifu Mungu kwa sababu ya maajabu ya uumbaji

    • Dunia itadumu milele (5)

    • Divai na mkate kwa ajili ya mwanadamu anayeweza kufa (15)

    • “Jinsi kazi zako zilivyo nyingi sana!” (24)

    • ‘Roho inapoondolewa, wanakufa’ (29)

104  Nafsi yangu na imsifu Yehova.+ Ee Yehova Mungu wangu, wewe ni mkuu sana.+ Umevaa utukufu* na fahari.+   Umejifunika nuru+ kama vazi;Unazitandaza mbingu kama kitambaa cha hema.+   Hujenga boriti za vyumba vyake vya juu katika maji yaliyo juu,*+Akiyafanya mawingu kuwa gari lake,+Akienda juu ya mabawa ya upepo.+   Huwafanya malaika wake kuwa roho,Wahudumu wake kuwa moto unaoteketeza kabisa.+   Ameiimarisha dunia juu ya misingi yake;+Haitasogezwa kutoka mahali pake* milele na milele.+   Uliifunika kwa vilindi vya maji kama kwa vazi.+ Maji yalisimama juu ya milima.   Kwa kemeo lako yalikimbia;+Kwa sauti ya mngurumo wako yalikimbia kwa wasiwasi   —Milima ilipanda+ na mabonde yakashuka—Mahali ulipokusudia yawepo.   Uliweka mpaka ambao hayapaswi kuvuka,+Ili yasiifunike dunia tena kamwe. 10  Wewe hupeleka chemchemi katika mabonde;*Kati ya milima zinatiririka. 11  Zinawapa maji wanyama wote wa mwituni;Punda mwitu hukata kiu yake. 12  Juu yake ndege wa angani hukaa;Wanaimba katikati ya majani mengi. 13  Anainywesha milima maji kutoka katika vyumba vyake vya juu.+ Dunia hushibishwa kwa matunda ya kazi zako.+ 14  Anaotesha majani kwa ajili ya ng’ombeNa mimea kwa ajili ya matumizi ya wanadamu,+Ili chakula kikue ardhini 15  Na divai inayofanya moyo wa mwanadamu ushangilie,+Mafuta yanayofanya uso ung’ae,Na mkate unaotegemeza moyo wa mwanadamu anayeweza kufa.+ 16  Miti ya Yehova imetosheka,Mierezi ya Lebanoni aliyopanda, 17  Ambamo ndege hutengeneza viota. Makao ya korongo+ ni miberoshi. 18  Milima mirefu ni ya mbuzi wa milimani;+Majabali ni kimbilio la wibari.+ 19  Ameuumba mwezi ili upime nyakati zilizowekwa;Jua linajua vizuri wakati wa kutua.+ 20  Wewe unaleta giza, usiku unaingia,+Wakati ambapo wanyama wote wa mwituni wanazunguka-zunguka. 21  Wanasimba* hunguruma ili wapate mawindo+Na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.+ 22  Jua linapochomoza,Wanarudi na kulala katika mapango yao. 23  Mwanadamu huenda kwenye kazi yake,Naye hufanya kazi kwa jasho mpaka jioni. 24  Jinsi kazi zako zilivyo nyingi sana, Ee Yehova!+ Umezifanya zote kwa hekima.+ Dunia imejaa vitu ulivyoumba. 25  Kisha kuna bahari, ni kubwa sana na pana,Imejaa viumbe walio hai wasio na idadi, wadogo kwa wakubwa.+ 26  Humo meli husafiri,Na Lewiathani,*+ uliyemuumba ili acheze humo. 27  Wote wanakungojea weweUwape chakula chao kwa wakati wake.+ 28  Wanakusanya unachowapa.+ Unapofumbua mkono wako, wanashiba vitu vyema.+ 29  Ukiuficha uso wako, wanahangaika. Ukiiondoa roho yao, wanakufa na kurudi mavumbini.+ 30  Ukiituma roho yako, wanaumbwa,+Nawe unaifanya ardhi iwe na sura mpya. 31  Utukufu wa Yehova utadumu milele. Yehova atashangilia kwa sababu ya kazi zake.+ 32  Huitazama dunia, inatetemeka;Huigusa milima, inafuka moshi.+ 33  Nitamwimbia Yehova+ maisha yangu yote;Nitamwimbia sifa* Mungu wangu maadamu ninaishi.+ 34  Mawazo yangu na yampendeze.* Nitashangilia kwa sababu ya Yehova. 35  Watenda dhambi watatoweka duniani,Na waovu hawatakuwapo tena.+ Nafsi yangu na imsifu Yehova. Msifuni Yah!*

Maelezo ya Chini

Au “adhama.”
Tnn., “katika maji.”
Au “Haitatikiswa.”
Au “makorongo.”
Au “Wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Angalia Kamusi.
Au “Nitampigia muziki.”
Au labda, “Kutafakari kwangu kumhusu na kupendeze.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.