Zaburi 106:1-48

  • Waisraeli wakosa kuthamini

    • Walisahau haraka matendo ya Mungu (13)

    • Walibadili utukufu wa Mungu kwa mfano wa ng’ombe dume (19, 20)

    • Hawakuwa na imani katika ahadi ya Mungu (24)

    • Walijiunga na ibada ya Baali (28)

    • Watoto watolewa dhabihu kwa roho waovu (37)

106  Msifuni Yah!* Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+   Ni nani anayeweza kutangaza kikamili matendo ya Yehova yenye nguvuAu kutangaza matendo yake yote yanayostahili sifa?+   Wenye furaha ni wale wanaotenda haki,Ambao sikuzote wanatenda yaliyo sawa.+   Nikumbuke, Ee Yehova, unapowaonyesha kibali* watu wako.+ Nitunze kwa matendo yako ya wokovu,   Ili nifurahie wema unaowaonyesha watu wako uliowachagua,+Ili nishangilie pamoja na taifa lako,Ili nikusifu kwa fahari* pamoja na urithi wako.   Tumetenda dhambi kama mababu zetu;+Tumetenda kosa; tumetenda uovu.+   Mababu zetu kule Misri hawakuthamini* kazi zako zinazostaajabisha. Hawakukumbuka upendo wako mwingi mshikamanifu,Bali waliasi baharini, kando ya Bahari Nyekundu.+   Lakini aliwaokoa kwa ajili ya jina lake,+Ili kufanya nguvu zake zijulikane.+   Aliikemea Bahari Nyekundu, ikakauka;Aliwaongoza katika vilindi vyake kana kwamba wanapitia jangwani;*+ 10  Aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui yao+Na kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.+ 11  Maji yaliwafunika maadui wao;Hakuna hata mmoja wao aliyeokoka.*+ 12  Kisha wakawa na imani katika ahadi yake;+Wakaanza kuimba sifa yake.+ 13  Lakini walisahau haraka mambo aliyotenda;+Hawakungojea ushauri wake. 14  Walifuata tamaa zao za kichoyo nyikani;+Walimjaribu Mungu jangwani.+ 15  Aliwapa walichoomba,Lakini akawapiga kwa ugonjwa uliowadhoofisha.+ 16  Walimwonea wivu Musa kambiniNa Haruni,+ mtakatifu wa Yehova.+ 17  Kisha dunia ikafunguka na kummeza DathaniNa kuwafunika wale waliokusanyika pamoja na Abiramu.+ 18  Moto uliwaka katika kundi lao;Mwali wa moto ukawateketeza kabisa waovu.+ 19  Walitengeneza ndama kule HorebuNa kuiinamia sanamu ya chuma;*+ 20  Waliubadili utukufu wanguKwa mfano wa ng’ombe dume anayekula nyasi.+ 21  Walimsahau Mungu+ Mwokozi wao,Aliyetenda mambo makuu nchini Misri,+ 22  Kazi zinazostaajabisha katika nchi ya Hamu,+Mambo yanayoogopesha kwenye Bahari Nyekundu.+ 23  Alikuwa karibu kuamuru waangamizwe,Lakini Musa, mchaguliwa wake, akaingilia kati*Ili kuzuia hasira yake inayoangamiza.+ 24  Kisha wakaidharau ile nchi inayotamanika;+Hawakuwa na imani katika ahadi yake.+ 25  Waliendelea kunung’unika katika mahema yao;+Hawakuisikiliza sauti ya Yehova.+ 26  Kwa hiyo akainua mkono wake na kuapa kuwahusuKwamba angewaangusha nyikani;+ 27  Angewaangusha wazao wao miongoni mwa mataifa,Naye angewatawanya katika nchi mbalimbali.+ 28  Kisha wakajiunga* na ibada ya Baali wa Peori,+Nao wakala dhabihu zilizotolewa kwa waliokufa.* 29  Walimkasirisha kwa matendo yao,+Na pigo likazuka miongoni mwao.+ 30  Lakini Finehasi alipoinuka na kuingilia kati,Pigo hilo lilikomeshwa.+ 31  Na jambo hilo likahesabiwa kwake kuwa uadilifu Katika vizazi vyote milele.+ 32  Walimkasirisha kwenye maji ya Meriba,*Na mambo yakamwendea Musa vibaya kwa sababu yao.+ 33  Waliitia uchungu roho yake,Naye akaongea bila kufikiri kwa midomo yake.+ 34  Hawakuyaangamiza mataifa,+Kama Yehova alivyokuwa amewaamuru.+ 35  Lakini walichangamana na mataifa hayo+Na kuzikubali* njia zao.+ 36  Waliendelea kuabudu sanamu zao,+Nazo zikawa mtego kwao.+ 37  Waliwatoa dhabihu wana waoNa mabinti wao kwa roho waovu.+ 38  Waliendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+Damu ya wana wao na mabinti wao wenyeweAmbao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+ Na nchi ikachafuliwa kwa umwagaji wa damu. 39  Wakawa wachafu kwa sababu ya kazi zao;Walifanya ukahaba wa kiroho kwa matendo yao.+ 40  Kwa hiyo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya watu wake,Naye akauchukia sana urithi wake. 41  Aliwatia tena na tena mikononi mwa mataifa,+Ili wale waliowachukia waweze kuwatawala.+ 42  Maadui wao waliwakandamiza,Nao wakatiishwa chini ya nguvu zao.* 43  Aliwaokoa mara nyingi,+Lakini walikuwa wakiasi na kukosa kutii,+Nao walikuwa wakifedheheshwa kwa sababu ya makosa yao.+ 44  Lakini alikuwa akiona taabu yao+Na kusikia kilio chao cha kuomba msaada.+ 45  Na kwa ajili yao alikuwa akikumbuka agano lake,Naye alikuwa akiwahurumia,* akichochewa na upendo wake mwingi* mshikamanifu.+ 46  Alikuwa akisababisha wahurumiweNa wote waliowachukua mateka.+ 47  Tuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+Na kutukusanya kutoka katika mataifa+Ili tulishukuru jina lako takatifuNa tushangilie kukusifu wewe.*+ 48  Yehova, Mungu wa Israeli, na asifiweKwa umilele wote.*+ Na watu wote waseme, “Amina!”* Msifuni Yah!*

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “nia njema.”
Au “nijigambe kukuhusu.”
Au “hawakuelewa maana ya.”
Au “nyikani.”
Au “aliyebaki.”
Au “sanamu ya kuyeyushwa.”
Tnn., “akasimama kwenye pengo hilo mbele zake.”
Au “wakashikamana.”
Yaani, dhabihu zilizotolewa kwa watu waliokufa au kwa miungu ambayo haina uhai.
Maana yake “Kugombana.”
Au “kujifunza.”
Tnn., “mkono wao.”
Au “akighairi.”
Au “mkubwa; mkuu.”
Au “tupate shangwe kwa kukusifu.”
Au “Milele na milele.”
Au “Na iwe hivyo!”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.