Zaburi 107:1-43

  • Mshukuruni Mungu kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha

    • Aliwaongoza katika njia inayofaa (7)

    • Aliwatosheleza wenye kiu na wenye njaa (9)

    • Aliwatoa gizani (14)

    • Alituma neno lake kuwaponya (20)

    • Huwalinda maskini ili wasikandamizwe (41)

107  Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+   Wale waliokombolewa* na Yehova na waseme jambo hilo,Wale aliowakomboa kutoka mikononi mwa* adui,+   Wale aliowakusanya pamoja kutoka katika nchi mbalimbali,+Kutoka mashariki na kutoka magharibi,*Kutoka kaskazini na kutoka kusini.+   Walitangatanga nyikani, jangwani;Hawakupata njia ya kwenda katika jiji ambamo wangeweza kuishi.   Walikuwa na njaa na kiu;Walidhoofika kwa sababu ya uchovu.   Waliendelea kumlilia Yehova walipokuwa wakitaabika;+Aliwaokoa kutoka katika dhiki yao.+   Aliwaongoza kutembea katika njia inayofaa+Ili wafike katika jiji ambamo wangeweza kuishi.+   Watu na wamshukuru Yehova+ kwa sababu ya upendo wake mshikamanifuNa kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.+   Kwa maana amewatosheleza wenye kiu*Na kuwashibisha wenye njaa* kwa vitu vyema.+ 10  Baadhi yao walikuwa wakiishi katika giza zito sana,Wafungwa walioteseka na kufungwa kwa vyuma. 11  Kwa maana walikuwa wameliasi neno la Mungu;Waliudharau ushauri wa Aliye Juu Zaidi.+ 12  Kwa hiyo aliinyenyekeza mioyo yao kupitia taabu;+Walijikwaa, na hakukuwa na yeyote wa kuwasaidia. 13  Walimlilia Yehova awasaidie walipokuwa wakitaabika;Akawaokoa kutoka katika dhiki yao. 14  Aliwatoa katika giza zito sana,Na kuzikata pingu zao.+ 15  Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifu+Na kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu. 16  Kwa maana ameivunja milango ya shabaNa kuyakata makomeo ya chuma.+ 17  Walikuwa wapumbavu, nao wakateseka+Kwa sababu ya makosa yao na dhambi zao.+ 18  Walipoteza hamu ya kula kila aina ya chakula;*Waliyakaribia malango ya kifo. 19  Walikuwa wakimlilia Yehova awasaidie walipokuwa wakitaabika;Naye alikuwa akiwaokoa kutoka katika dhiki yao. 20  Alikuwa akituma neno lake na kuwaponya+Na kuwaokoa kutoka katika mashimo ambamo walikuwa wamenaswa. 21  Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifuNa kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu. 22  Na watoe dhabihu za shukrani+Na kutangaza kazi zake kwa kilio cha shangwe. 23  Wale wanaosafiri kwa meli baharini,Wanaofanya biashara yao kwenye maji mengi,+ 24  Wameziona kazi za YehovaNa kazi zake zinazostaajabisha zilizo vilindini;+ 25  Jinsi dhoruba ya upepo inavyoinuka kwa neno lake,+Na kuyainua mawimbi ya bahari. 26  Hayo huinuka juu angani;Hushuka chini kwa nguvu vilindini. Ujasiri wao* huyeyuka kwa sababu ya msiba unaokaribia. 27  Wao hugaagaa na kupepesuka kama mlevi,Na ustadi wao wote unakosa manufaa kabisa.+ 28  Kisha wanamlilia Yehova kwa sauti wanapotaabika,+Naye huwaokoa kutoka katika dhiki yao. 29  Yeye huituliza dhoruba ya upepo;Mawimbi ya bahari hunyamaza.+ 30  Wanashangilia yanapotulia,Naye huwaongoza kwenda kwenye bandari wanayotamani. 31  Watu na wamshukuru Yehova kwa sababu ya upendo wake mshikamanifuNa kwa sababu ya kazi zake zinazostaajabisha anazowatendea wanadamu.+ 32  Na wamkweze katika kutaniko la watu,+Na wamsifu katika baraza la* wazee. 33  Yeye hubadili mito kuwa jangwa,Na chemchemi za maji kuwa ardhi iliyokauka,+ 34  Nchi inayozaa kuwa nchi iliyoharibika yenye chumvi,+Kwa sababu ya uovu wa wale wanaokaa humo. 35  Yeye hulibadili jangwa kuwa madimbwi ya maji yenye matete,Na nchi kavu kuwa chemchemi za maji.+ 36  Huwafanya wenye njaa wakae humo,+Ili wajenge jiji ambamo wanaweza kuishi.+ 37  Wanapanda mbegu mashambani na kupanda mashamba ya mizabibu+Yanayozaa mazao mengi.+ 38  Huwabariki, nao huongezeka sana;Haachi ng’ombe wao wapungue.+ 39  Kisha wanakuwa wachache tena na kuaibishwaKwa sababu ya ukandamizaji, msiba, na huzuni. 40  Huwamwagia wakuu dharauNa kuwafanya watangetange jangwani kusiko na njia.+ 41  Lakini huwalinda* maskini ili wasikandamizwe+Na kufanya familia zao ziwe nyingi kama kundi la kondoo. 42  Wanyoofu huona hilo na kushangilia;+Lakini waovu wote hufunga vinywa vyao.+ 43  Yeyote aliye na hekima atayachunguza mambo hayo+Naye atatafakari kwa makini matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu.+

Maelezo ya Chini

Au “walionunuliwa.”
Au “katika nguvu za.”
Au “Kutoka mapambazuko ya jua na kutoka machweo ya jua.”
Au “amezitosheleza nafsi zilizokauka.”
Au “kuzishibisha nafsi zenye njaa.”
Au “Walichukia kabisa vyakula vyote.”
Au “Nafsi yao.”
Tnn., “kwenye kiti cha.”
Au “huwainua juu,” yaani, ili wasifikiwe.