Zaburi 108:1-13

  • Sala ya ushindi dhidi ya maadui

    • Wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote (12)

    • “Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu” (13)

Wimbo. Muziki wa Daudi. 108  Moyo wangu uko imara, Ee Mungu. Nitaimba na kupiga muziki kwa nafsi yangu yote.*+   Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.+ Nitayaamsha mapambazuko.   Nitakusifu miongoni mwa mataifa, Ee Yehova,Nami nitakuimbia sifa* miongoni mwa mataifa.   Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+Na uaminifu wako, unafika mpaka angani.   Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+   Ili wapendwa wako waokolewe,Tuokoe kwa mkono wako wa kuume na unijibu.+   Mungu ameongea katika utakatifu wake:* “Nitashangilia, nitawagawia Shekemu+ kuwa urithi,Nami nitawapimia Bonde la* Sukothi.+   Gileadi+ ni yangu, na Manase ni yangu,Na Efraimu ni kofia ya kukinga* kichwa changu;+Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+   Moabu ni beseni langu la kuogea.+ Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+ Nitapaza sauti kwa ushindi juu ya Ufilisti.”+ 10  Ni nani atakayenipeleka kwenye lile jiji lenye ngome? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+ 11  Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetukataa,Mungu wetu, ambaye haendi tena na majeshi yetu?+ 12  Tusaidie katika taabu yetu,+Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote.+ 13  Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu,+Naye atawakanyagia chini maadui wetu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “hata kwa utukufu wangu.”
Au “nitakupigia muziki.”
Au labda, “mahali pake patakatifu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Tnn., “ngome ya.”