Zaburi 11:1-7

  • Kumkimbilia Yehova

    • “Yehova yumo katika hekalu lake takatifu” (4)

    • Mungu humchukia yeyote anayependa ukatili (5)

Kwa kiongozi. Wa Daudi. 11  Nimemkimbilia Yehova.+ Basi mnawezaje kuniambia:* “Kimbilia kwenye mlima wako kama ndege!   Tazama jinsi waovu wanavyoukunja upinde;Huutia mshale wao kwenye kamba ya upinde,Ili wawapige kutoka gizani wale walio wanyoofu moyoni.   Misingi* inapobomolewa,Mtu mwadilifu anaweza kufanya nini?”   Yehova yumo katika hekalu lake takatifu.+ Kiti cha ufalme cha Yehova kiko mbinguni.+ Macho yake mwenyewe yanatazama, macho yake yaliyo makini* yanawachunguza wanadamu.+   Yehova humchunguza mwadilifu na pia mwovu;+Humchukia* mtu yeyote anayependa ukatili.+   Atawanyeshea waovu mitego;*Moto na kiberiti+ na upepo unaounguza vitakuwa fungu la kikombe chao.   Kwa maana Yehova ni mwadilifu;+ yeye hupenda matendo ya uadilifu.+ Wanyoofu watauona uso wake.*+

Maelezo ya Chini

Au “kuiambia nafsi yangu.”
Au “Misingi ya haki.”
Au “yanayong’aa.”
Au “Nafsi yake inamchukia; Yeye binafsi anamchukia.”
Au labda, “makaa ya mawe yanayowaka.”
Au “watajionea kibali chake.”