Zaburi 110:1-7

  • Mfalme na kuhani kama Melkizedeki

    • ‘Tawala kati ya maadui wako’ (2)

    • Vijana wanaojitoa kwa hiari ni kama matone ya umande (3)

Muziki wa Daudi. 110  Yehova alimtangazia hivi Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume+Mpaka nitakapowaweka maadui wako kuwa kiti cha miguu yako.”+   Yehova atainyoosha fimbo ya ufalme ya nguvu zako kutoka Sayuni, akisema: “Nenda ukitiisha kati ya maadui wako.”+   Watu wako watajitoa kwa hiari katika siku ya jeshi lako.* Katika utakatifu wenye fahari, kutoka katika tumbo la uzazi la mapambazuko,Una kundi lako la vijana kama matone ya umande.   Yehova ameapa naye hatabadili nia yake:* “Wewe ni kuhani milele+Kwa mfano wa Melkizedeki!”+   Yehova atakuwa kwenye mkono wako wa kulia;+Atawaponda wafalme katika siku ya hasira yake.+   Atatekeleza hukumu dhidi ya* mataifa;+Atajaza maiti nchini.+ Atamponda kiongozi wa* nchi kubwa sana.*   Atakunywa* maji ya kijito kilicho kando ya barabara. Kwa hiyo, atakiinua juu kichwa chake.

Maelezo ya Chini

Au “siku ambayo jeshi lako litakusanyika.”
Au “hataghairi.”
Au “miongoni mwa.”
Tnn., “Ataponda kichwa cha.”
Au “dunia nzima.”
Anayerejelewa ni “Bwana wangu” anayetajwa katika mstari wa 1.