Zaburi 112:1-10

  • Mwadilifu humwogopa Yehova

    • Mtu anayekopesha kwa ukarimu atafanikiwa (5)

    • “Mwadilifu atakumbukwa milele” (6)

    • Mtu mkarimu huwapa maskini (9)

112  Msifuni Yah!*+ א [Aleph] Mwenye furaha ni mtu anayemwogopa Yehova,+ב [Beth] Anayependezwa sana na amri zake.+ ג [Gimel]   Wazao wake watakuwa wenye nguvu duniani,ד [Daleth] Na kizazi cha mtu mnyoofu kitabarikiwa.+ ה [He]   Nyumbani mwake mna mali na utajiri,ו [Waw] Na uadilifu wake unadumu milele. ז [Zayin]   Yeye humwangazia mnyoofu kama nuru gizani.+ ח [Heth] Ni mwenye huruma* na mwenye rehema+ na ni mwadilifu. ט [Teth]   Mambo humwendea vema mtu anayekopesha kwa ukarimu.*+ י [Yod] Hufanya mambo yake kwa haki. כ [Kaph]   Hatatikiswa kamwe.+ ל [Lamed] Mwadilifu atakumbukwa milele.+ מ [Mem]   Hataogopa habari mbaya.+ נ [Nun] Moyo wake ni imara, unamtumaini Yehova.+ ס [Samekh]   Moyo wake hauwezi kutikiswa;* haogopi;+ע [Ayin] Hatimaye atawatazama maadui wake wakishindwa.+ פ [Pe]   Amegawa kwa wingi;* amewapa maskini.+ צ [Tsade] Uadilifu wake unadumu milele.+ ק [Qoph] Nguvu zake mwenyewe zitakwezwa* kwa utukufu. ר [Resh] 10  Mwovu ataona na kukasirika. ש [Shin] Atasaga meno yake na kuyeyuka. ת [Taw] Tamaa za mwovu zitaangamia.+

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “neema.”
Au “fadhili.”
Au “ni thabiti; ni imara.”
Au “kwa ukarimu.”
Tnn., “Pembe yake mwenyewe itakwezwa.”