Zaburi 113:1-9

  • Mungu aliye juu humwinua mtu wa hali ya chini

    • Jina la Yehova lasifiwa milele (2)

    • Mungu huinama chini (6)

113  Msifuni Yah!* Msifuni, enyi watumishi wa Yehova,Lisifuni jina la Yehova.   Jina la Yehova na lisifiweKuanzia sasa mpaka milele.+   Kuanzia jua linapochomoza mpaka linapotua,Jina la Yehova na lisifiwe.+   Yehova yuko juu zaidi ya mataifa yote;+Utukufu wake uko juu ya mbingu.+   Ni nani aliye kama Yehova Mungu wetu,+Anayekaa juu?*   Huinama chini ili atazame mbingu na dunia,+   Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka mavumbini. Humwinua juu maskini kutoka kwenye rundo la majivu*+   Ili amketishe pamoja na viongozi,Pamoja na viongozi wa watu wake.   Humpa makao mwanamke tasaKama mama mwenye furaha aliye na watoto.*+ Msifuni Yah!*

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Anayeketi juu kwenye kiti cha ufalme?”
Au labda, “jaa la takataka.”
Tnn., “wana.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.