Zaburi 114:1-8

  • Waisraeli wakombolewa kutoka Misri

    • Bahari ilikimbia (5)

    • Milima ilirukaruka kama kondoo dume (6)

    • Mwamba mgumu wabadilishwa kuwa chemchemi za maji (8)

114  Israeli alipotoka Misri,+Nyumba ya Yakobo ilipotoka kati ya watu waliozungumza lugha ya kigeni,   Yuda ikawa mahali pake patakatifu,Israeli, miliki yake.+   Bahari iliona hilo na kukimbia;+Mto Yordani ukarudi nyuma.+   Milima ilirukaruka kama kondoo dume,+Vilima, kama wanakondoo.   Ee bahari, ni nini kilichofanya ukimbie?+ Ee Yordani, kwa nini ulirudi nyuma?+   Enyi milima, kwa nini mlirukaruka kama kondoo dume,Kama wanakondoo, enyi vilima?   Tetemeka, Ee dunia, kwa sababu ya Bwana,Kwa sababu ya Mungu wa Yakobo,+   Anayeubadili mwamba kuwa dimbwi la maji lenye matete,Mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.+

Maelezo ya Chini