Zaburi 116:1-19

  • Wimbo wa shukrani

    • “Nitamlipa Yehova nini?” (12)

    • “Nitakiinua kikombe cha wokovu” (13)

    • “Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu” (14, 18)

    • Kifo cha washikamanifu kina thamani (15)

116  Ninampenda YehovaKwa sababu yeye huisikia* sauti yangu, sihi zangu za kuomba msaada.+   Kwa maana yeye hunitegea sikio lake,*+Nami nitamlilia maadamu ninaishi.*   Kamba za kifo zilinizunguka;Kaburi lilinishika kwa nguvu.*+ Nililemewa na taabu na huzuni.+   Lakini nikaliita jina la Yehova:+ “Ee, Yehova, niokoe!”*   Yehova ni mwenye huruma* na ni mwadilifu;+Mungu wetu ni mwenye rehema.+   Yehova anawalinda wasio na uzoefu.+ Nilishushwa chini, akaniokoa.   Acha nafsi* yangu ipumzike tena,Kwa maana Yehova amenitendea kwa fadhili.   Umeniokoa* kutoka katika kifo,Jicho langu kutokana na machozi, mguu wangu usijikwae.+   Nitatembea mbele za Yehova katika nchi ya walio hai. 10  Nilikuwa na imani, ndio maana niliongea;+Niliteseka sana. 11  Basi nikashikwa na hofu na kusema: “Kila mwanadamu ni mwongo.”+ 12  Nitamlipa Yehova niniKwa mema yote aliyonitendea? 13  Nitakiinua kikombe cha wokovu,*Nami nitaliitia jina la Yehova. 14  Nitamtimizia Yehova nadhiri zanguMbele ya watu wake wote.+ 15  Ni chenye thamani sana* machoni pa YehovaKifo cha washikamanifu wake.+ 16  Ninakusihi, Ee Yehova,Kwa maana mimi ni mtumishi wako. Mimi ni mtumishi wako, mwana wa kijakazi wako. Umezifungua pingu zangu.+ 17  Nitakutolea dhabihu ya shukrani;+Nitaliitia jina la Yehova. 18  Nitamtimizia Yehova nadhiri zangu+Mbele ya watu wake wote,+ 19  Katika nyua za nyumba ya Yehova,+Kati yako, Ee Yerusalemu. Msifuni Yah!*+

Maelezo ya Chini

Au labda, “Ninapenda kwa sababu Yehova huisikia.”
Au “huinama chini ili kunisikiliza.”
Tnn., “katika siku zangu.”
Tnn., “Nilipatwa na taabu za Sheoli.”
Au “iokoe nafsi yangu.”
Au “neema.”
Angalia Kamusi.
Au “Umeiokoa nafsi yangu.”
Au “wokovu mkuu.”
Au “Ni cha bei kubwa sana.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.