Zaburi 118:1-29

  • Kushukuru kwa sababu ya ushindi wa Yehova

    • ‘Nilimlilia Yah, naye akanijibu’ (5)

    • “Yehova yuko upande wangu” (6, 7)

    • Jiwe lililokataliwa litakuwa jiwe kuu la pembeni (22)

    • “Yule anayekuja katika jina la Yehova” (26)

118  Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.   Watu wa Israeli na waseme sasa: “Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”   Watu wa nyumba ya Haruni na waseme sasa: “Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”   Wale wanaomwogopa Yehova na waseme sasa: “Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”   Nilimlilia Yah* nilipokuwa nikitaabika;Yah akanijibu na kunipeleka mahali salama.*+   Yehova yuko upande wangu; sitaogopa.+ Mwanadamu atanifanya nini?+   Yehova yuko upande wangu akiwa msaidizi wangu;*+Wale wanaonichukia nitawatazama wakishindwa.+   Ni bora kumkimbilia YehovaKuliko kuwatumaini wanadamu.+   Ni bora kumkimbilia YehovaKuliko kuwatumaini wakuu.+ 10  Mataifa yote yalinizingira,Lakini katika jina la Yehova,Niliyafukuza.+ 11  Yalinizingira, naam, yalinizingira kabisa,Lakini katika jina la Yehova,Niliyafukuza. 12  Yalinizingira kama nyuki,Lakini yalizimwa haraka kama moto unaoteketeza miiba. Katika jina la Yehova,Niliyafukuza.+ 13  Nilisukumwa kwa nguvu* ili nianguke,Lakini Yehova alinisaidia. 14  Yah ni mahali pangu pa kujificha na nguvu zangu,Naye amekuwa wokovu wangu.+ 15  Sauti ya shangwe na wokovu*Imo katika mahema ya waadilifu. Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+ 16  Mkono wa kuume wa Yehova unajikweza;Mkono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+ 17  Sitakufa, hapana, nitaishi,Ili nizitangaze kazi za Yah.+ 18  Yah aliniadhibu vikali,+Lakini hakunitia mikononi mwa kifo.+ 19  Nifungulieni malango ya uadilifu;+Nitaingia humo na kumsifu Yah. 20  Hili ndilo lango la Yehova. Waadilifu wataingia humo.+ 21  Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+Nawe ukawa wokovu wangu. 22  Jiwe ambalo wajenzi walilikataaLimekuwa jiwe kuu la pembeni.*+ 23  Hili limetoka kwa Yehova;+Linastaajabisha machoni petu.+ 24  Hii ndiyo siku ambayo Yehova ameifanya;Tutaishangilia na kuifurahia. 25  Yehova, tuokoe, tafadhali, tunakusihi! Yehova, tupe ushindi, tafadhali! 26  Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova;+Tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yehova. 27  Yehova ni Mungu;Hutupatia nuru.+ Mkiwa na matawi mikononi jiungeni na maandamano ya sherehe,+Mpaka kwenye pembe za madhabahu.+ 28  Wewe ni Mungu wangu, nami nitakusifu;Mungu wangu, nitakukweza.+ 29  Mshukuruni Yehova,+ kwa maana yeye ni mwema;Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+

Maelezo ya Chini

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “mahali penye nafasi kubwa.”
Au labda, “pamoja na wale wanaonisaidia.”
Au labda, “Ulinisukuma kwa nguvu.”
Au “ushindi.”
Tnn., “kichwa cha pembeni.”