Zaburi 12:1-8

  • Yehova ainuka ili kutenda

    • Maneno ya Mungu ni safi (6)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na sauti ya Sheminithi.* Muziki wa Daudi. 12  Niokoe, Ee Yehova, kwa maana mtu mshikamanifu hayupo tena;Watu waaminifu wametoweka kutoka miongoni mwa wanadamu.   Wanaambiana uwongo;Wanasifusifu kwa midomo yao* na kuzungumza kwa mioyo midanganyifu.*+   Yehova ataikata kabisa midomo yote inayosifusifuNa ulimi unaojigamba kupindukia,+   Wale wanaosema: “Tutashinda kwa ndimi zetu. Tunatumia midomo yetu tupendavyo;Ni nani atakayekuwa bwana mkubwa wetu?”+   “Kwa sababu wale wanaoteswa wanakandamizwa,Kwa sababu ya kilio cha uchungu cha maskini,+Nitainuka na kutenda,” asema Yehova. “Nitawaokoa kutoka kwa wale wanaowatendea kwa dharau.”*   Maneno ya Yehova ni safi;+Ni kama fedha iliyosafishwa katika tanuru la udongo,* iliyosafishwa mara saba.   Utawalinda, Ee Yehova;+Utamlinda kila mmoja wao milele kutokana na kizazi hiki.   Waovu wanatembea huku na huku kwa uhuruKwa sababu wanadamu wanaendeleza upotovu.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Tnn., “Wanaongea kwa mdomo laini.”
Tnn., “kwa moyo na moyo.”
Au “wanaojitutumua mbele yao.”
Au labda, “tanuru la kuyeyusha lililowekwa ardhini.”