Zaburi 120:1-7

  • Mgeni atamani amani

    • ‘Niokoe kutoka kwa ulimi mdanganyifu’ (2)

    • “Mimi ni mtu wa amani” (7)

Wimbo wa Safari za Kupanda.* 120  Nilimwita Yehova nilipokuwa nikitaabika,+Naye akanijibu.+   Ee Yehova, niokoe kutoka kwa midomo inayosema uwongoNa kutoka kwa ulimi mdanganyifu.   Mungu atakufanya nini, Naye atakuadhibu jinsi gani,*Ewe ulimi mdanganyifu?+   Kwa mishale mikali+ ya shujaaNa makaa yanayowaka moto+ ya miretemu.   Ole wangu, kwa maana nimeishi kama mgeni Mesheki!+ Nimekuwa nikiishi kati ya mahema ya Kedari.+   Nimekuwa nikiishi mbali kwa muda mrefuPamoja na watu wanaochukia amani.+   Mimi ni mtu wa amani, lakini ninapoongea,Wao wanataka vita.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Tnn., “Naye atakuongezea nini?”