Zaburi 121:1-8

  • Yehova huwalinda watu wake

    • “Msaada wangu hutoka kwa Yehova” (2)

    • Yehova halali usingizi kamwe (3, 4)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 121  Ninayainua macho yangu nitazame milimani.+ Msaada wangu utatoka wapi?   Msaada wangu hutoka kwa Yehova,+Muumba wa mbingu na dunia.   Hataruhusu kamwe mguu wako uteleze.*+ Yeye anayekulinda hatasinzia kamwe.   Tazama! Hatasinzia kamwe wala kulala usingizi,Yeye anayelinda Israeli.+   Yehova anakulinda. Yehova ni kivuli+ kwenye mkono wako wa kulia.+   Mchana, jua halitakuchoma,+Wala mwezi usiku.+   Yehova atakulinda dhidi ya madhara yote.+ Ataulinda uhai wako.*+   Yehova atakulinda katika mambo yote unayofanya*Kuanzia sasa mpaka milele.

Maelezo ya Chini

Au “uyumbe.”
Au “Atailinda nafsi yako.”
Tnn., “unapotoka nje na unapoingia ndani.”