Zaburi 122:1-9

  • Sala ya kuomba jiji la Yerusalemu liwe na amani

    • Shangwe ya kwenda katika nyumba ya Yehova (1)

    • Jiji lililounganishwa pamoja kama kitu kimoja (3)

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi. 122  Nilishangilia waliponiambia: “Na twende katika nyumba ya Yehova.”+   Na sasa miguu yetu imesimamaNdani ya malango yako, Ee Yerusalemu.+   Yerusalemu limejengwa kama jijiAmbalo limeunganishwa pamoja kama kitu kimoja.+   Makabila yamepanda kwenda humo,Makabila ya Yah,*Kulingana na kikumbusho walichopewa Waisraeli,Ili walishukuru jina la Yehova.+   Kwa maana viti vya ufalme vya hukumu viliwekwa huko,+Viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.+   Ombeni ili Yerusalemu liwe na amani.+ Wale wanaokupenda, Ee jiji, watakuwa salama.   Amani na idumu ndani ya maboma yako,*Usalama ndani ya minara yako yenye ngome.   Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu nitasema: “Amani na iwe ndani yako.”   Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu,+Nitakutakia mema.

Maelezo ya Chini

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “kuta zako zenye ngome.”