Zaburi 124:1-8
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
124 “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi”+
—Watu wa Israeli na waseme sasa—
2 “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi+Watu walipokuja kutushambulia,+
3 Basi wangetumeza tukiwa hai+Hasira yao ilipokuwa ikiwaka dhidi yetu.+
4 Kisha maji yangetufagilia mbali,Mafuriko yangetufunika.+
5 Maji yenye nguvu yangetulemea.
6 Yehova na asifiwe,Kwa maana hakututia katika meno yao kama mawindo.
7 Sisi* ni kama ndege aliyeponyokaKutoka katika mtego wa mwindaji;+Mtego ulivunjika,Nasi tukaponyoka.+
8 Msaada wetu uko katika jina la Yehova,+Muumba wa mbingu na dunia.”
Maelezo ya Chini
^ Au “Nafsi yetu.”