Zaburi 125:1-5
Wimbo wa Safari za Kupanda.
125 Wale wanaomtumaini Yehova+Ni kama Mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikiswaBali hudumu milele.+
2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,+Ndivyo Yehova anavyowazunguka watu wake+Kuanzia sasa mpaka milele.
3 Fimbo ya ufalme ya uovu haitadumu katika nchi waliyogawiwa waadilifu,+Ili waadilifu wasije wakatenda* jambo baya.+
4 Ee Yehova, watendee mema walio wema,+Walio wanyoofu moyoni mwao.+
5 Lakini wale wanaogeuka na kufuata njia zao zilizopotoka,Yehova atawaondoa pamoja na watenda maovu.+
Amani na iwe juu ya Israeli.
Maelezo ya Chini
^ Au “wasiielekeze mikono yao kutenda.”