Zaburi 125:1-5

  • Yehova huwalinda watu wake

    • “Kama milima inavyozunguka Yerusalemu” (2)

    • “Amani na iwe juu ya Israeli” (5)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 125  Wale wanaomtumaini Yehova+Ni kama Mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikiswaBali hudumu milele.+   Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,+Ndivyo Yehova anavyowazunguka watu wake+Kuanzia sasa mpaka milele.   Fimbo ya ufalme ya uovu haitadumu katika nchi waliyogawiwa waadilifu,+Ili waadilifu wasije wakatenda* jambo baya.+   Ee Yehova, watendee mema walio wema,+Walio wanyoofu moyoni mwao.+   Lakini wale wanaogeuka na kufuata njia zao zilizopotoka,Yehova atawaondoa pamoja na watenda maovu.+ Amani na iwe juu ya Israeli.

Maelezo ya Chini

Au “wasiielekeze mikono yao kutenda.”