Zaburi 126:1-6

  • Sayuni litarudishwa kwa shangwe

    • ‘Yehova ametenda mambo makuu’ (3)

    • Baada ya kutokwa na machozi, kutakuwa na shangwe (5, 6)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 126  Yehova alipowakusanya na kuwarudisha mateka wa Sayuni,+Tulifikiri tunaota ndoto.   Wakati huo kinywa chetu kilijaa kichekoNa ulimi wetu kelele za shangwe.+ Wakati huo ilisemwa miongoni mwa mataifa: “Yehova amewatendea mambo makuu.”+   Yehova ametutendea mambo makuu,+Nasi tuna shangwe nyingi sana.   Wakusanye na kuwarudisha watu wetu waliotekwa, Ee Yehova,Kama vijito vya Negebu.*   Wale wanaopanda mbegu kwa machoziWatavuna kwa kelele za shangwe.   Yule anayetoka kwenda nje, ingawa analia,Akiwa amebeba mfuko wake uliojaa mbegu,Kwa hakika atarudi kwa kelele za shangwe,+Akiwa amebeba masuke yake.+

Maelezo ya Chini

Au “makorongo ya kusini.”