Zaburi 128:1-6

  • Furaha kwa sababu ya kumwogopa Yehova

    • Mke kama mzabibu unaozaa matunda mengi (3)

    • “Na uone Yerusalemu likipata ufanisi” (5)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 128  Mwenye furaha ni kila mtu anayemwogopa Yehova,+Anayetembea katika njia Zake.+   Utakula mazao ambayo mkono wako ulifanya kazi ngumu kuyapata. Utakuwa na furaha na kufurahia ufanisi.+   Mke wako atakuwa kama mzabibu unaozaa matunda mengi nyumbani mwako;+Watoto wako watakuwa kama machipukizi ya mzeituni kuzunguka meza yako.   Tazama! Hivyo ndivyo mwanamume anayemwogopa YehovaAtakavyobarikiwa.+   Yehova atakubariki kutoka Sayuni. Na uone Yerusalemu likipata ufanisi sikuzote za maisha yako+   Na uone watoto wa watoto wako. Na amani iwe juu ya Israeli.

Maelezo ya Chini