Zaburi 13:1-6

  • Kutamani wokovu wa Yehova

    • ‘Mpaka lini, Ee Yehova?’ (1, 2)

    • Yehova huthawabisha kwelikweli (6)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 13  Ee Yehova, utanisahau mpaka lini? Milele? Utanificha uso wako mpaka lini?+   Nitahangaika kwa wasiwasi mpaka lini,Nikiwa na huzuni moyoni mwangu kila siku? Adui yangu atanishinda mpaka lini?+   Nitazame na unijibu, Ee Yehova Mungu wangu. Yatie nuru macho yangu, ili nisilale usingizi katika kifo,   Ili adui yangu asiseme: “Nimemshinda!” Usiruhusu wapinzani wangu washangilie kuanguka kwangu.+   Lakini mimi, ninautumaini upendo wako mshikamanifu;+Moyo wangu utashangilia kwa sababu ya matendo yako ya wokovu.+   Nitamwimbia Yehova, kwa maana amenithawabisha kwelikweli.*+

Maelezo ya Chini

Au “ameshughulika nami kwa njia inayothawabisha.”