Zaburi 132:1-18

  • Daudi achaguliwa na pia Sayuni

    • “Usimkatae mtiwa-mafuta wako” (10)

    • Makuhani wa Sayuni wavishwa wokovu (16)

Wimbo wa Safari za Kupanda. 132  Ee Yehova, mkumbuke DaudiNa mateso yake yote;+   Jinsi alivyomwapia Yehova,Jinsi alivyomwekea nadhiri hii Mwenye Nguvu wa Yakobo:+   “Sitaingia katika hema langu, nyumbani mwangu.+ Sitalala kwenye kochi langu, kitandani mwangu;   Sitayaruhusu macho yangu yalale usingizi,Wala kope zangu kusinzia   Mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yehova,Makao bora* kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+   Tazama! Tulisikia habari hizo huko Efratha;+Tulizipata katika mashamba yaliyo msituni.+   Na tuingie katika makao yake;*+Na tuiname chini kwenye kiti cha miguu yake.+   Inuka, Ee Yehova, uje mahali pako pa kupumzikia,+Wewe na Sanduku la nguvu zako.+   Makuhani wako na wavae uadilifu,Washikamanifu wako na wapaze sauti kwa shangwe. 10  Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako,Usimkatae* mtiwa-mafuta wako.+ 11  Yehova amemwapia Daudi;Kwa hakika hatakosa kutimiza neno lake: “Mmoja wa wazao wako,*Nitamfanya aketi kwenye kiti chako cha ufalme.+ 12  Wana wako wakilishika agano languNa vikumbusho vyangu ninavyowafundisha,+Wana wao piaWataketi kwenye kiti chako cha ufalme milele.”+ 13  Kwa maana Yehova amelichagua Sayuni;+Amelitamani liwe makao yake:+ 14  “Hapa ndipo mahali pangu pa kupumzikia milele;Nitakaa hapa,+ kwa maana nimepatamani. 15  Nitapabariki sana kwa vyakula;Nitawashibisha maskini wake kwa mikate.+ 16  Makuhani wake nitawavisha wokovu,+Na washikamanifu wake watapaza sauti kwa shangwe.+ 17  Huko nitazifanya nguvu za Daudi zikue.* Nimemtayarishia taa mtiwa-mafuta wangu.+ 18  Nitawavisha aibu maadui wake,Lakini taji lililo kwenye kichwa chake litasitawi.”+

Maelezo ya Chini

Au “Hema tukufu la ibada.”
Au “hema lake tukufu la ibada.”
Tnn., “Usiugeuze nyuma uso wa.”
Tnn., “Mmoja kutoka katika uzao wa tumbo lako.”
Tnn., “nitaifanya pembe ya Daudi ikue.”