Zaburi 135:1-21

  • Msifuni Yah kwa sababu ya ukuu wake

    • Ishara na miujiza dhidi ya Misri (8, 9)

    • “Jina lako linadumu milele” (13)

    • Sanamu zisizo na uhai (15-18)

135  Msifuni Yah!* Lisifuni jina la Yehova;Msifuni, enyi watumishi wa Yehova,+   Ninyi mnaosimama katika nyumba ya Yehova,Katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.+   Msifuni Yah, kwa maana Yehova ni mwema.+ Liimbieni sifa* jina lake, kwa maana linapendeza.   Kwa maana Yah amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe,Israeli awe mali yake ya pekee.*+   Kwa maana ninajua vizuri kwamba Yehova ni mkuu;Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu mingine yote.+   Yehova hufanya kila jambo apendalo+Mbinguni na duniani, baharini na katika vilindi vyote.   Huyafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia;Hutengeneza radi* kwa ajili ya mvua;Huutoa upepo katika maghala yake.+   Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,Wanadamu na wanyama pia.+   Alipeleka ishara na miujiza kati yako, Ee Misri,+Dhidi ya Farao na watumishi wake wote.+ 10  Aliyaangamiza mataifa mengi+Na kuwaua wafalme hodari+ 11  —Sihoni mfalme wa Waamori,+Ogu mfalme wa Bashani,+Na falme zote za Kanaani. 12  Aliitoa nchi yao kuwa urithi,Urithi kwa watu wake Waisraeli.+ 13  Ee Yehova, jina lako linadumu milele. Ee Yehova, umaarufu wako unadumu* katika vizazi vyote.+ 14  Kwa maana Yehova atawatetea* watu wake,+Naye atawahurumia* watumishi wake.+ 15  Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,Kazi ya mikono ya mwanadamu.+ 16  Zina kinywa, lakini haziwezi kuongea;+Zina macho, lakini haziwezi kuona; 17  Zina masikio, lakini haziwezi kusikia. Hazina pumzi vinywani mwake.+ 18  Watu wanaozitengeneza watakuwa kama sanamu hizo,+Na pia wote wanaozitumaini.+ 19  Ee nyumba ya Israeli, msifuni Yehova. Ee nyumba ya Haruni, msifuni Yehova. 20  Ee nyumba ya Lawi, msifuni Yehova.+ Enyi mnaomwogopa Yehova, msifuni Yehova. 21  Yehova na asifiwe kutoka Sayuni,+Yeye anayekaa Yerusalemu.+ Msifuni Yah!+

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “Lipigieni muziki.”
Au “mali yake anayothamini sana.”
Au labda, “malango.”
Au “Huufanya mvuke upande.”
Au “jina lako linadumu.” Tnn., “ukumbusho wako unadumu.”
Au “ataamua kesi ya.”
Au “ataghairi kuwahusu.”