Zaburi 136:1-26

  • Upendo mshikamanifu wa Yehova hudumu milele

    • Mbingu na dunia ziliumbwa kwa ustadi (5, 6)

    • Farao alikufa katika Bahari Nyekundu (15)

    • Mungu huwakumbuka walioshuka moyo (23)

    • Huwapa chakula viumbe wote walio hai (25)

136  Mshukuruni Yehova, kwa maana ni mwema;+Upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+   Mshukuruni Mungu wa miungu,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.   Mshukuruni Bwana wa mabwana,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.   Yeye peke yake ndiye anayetenda mambo makuu yanayostaajabisha,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+   Aliziumba mbingu kwa ustadi,*+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.   Aliitandaza dunia juu ya maji,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.   Aliiumba ile mianga mikubwa,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,   Jua litawale mchana,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele,   Mwezi na nyota zitawale usiku,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 10  Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 11  Aliwatoa Waisraeli kutoka kati yao,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele, 12  Kwa mkono wenye nguvu+ na mkono ulionyooshwa,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 13  Aliigawa Bahari Nyekundu sehemu mbili,*+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 14  Aliwavusha Waisraeli katikati yake,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 15  Alimkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 16  Aliwaongoza watu wake kupitia nyikani,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 17  Aliwaua wafalme wakuu,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 18  Aliwaua wafalme hodari,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 19  Sihoni+ mfalme wa Waamori,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele, 20  Na Ogu+ mfalme wa Bashani,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 21  Aliitoa nchi yao kuwa urithi,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 22  Urithi kwa Israeli mtumishi wake,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 23  Alitukumbuka tulipokuwa wanyonge,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.+ 24  Alituokoa tena na tena kutoka kwa maadui wetu,+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 25  Huwapa chakula viumbe wote walio hai,*+Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele. 26  Mshukuruni Mungu wa mbinguni,Kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele.

Maelezo ya Chini

Au “kwa uelewaji.”
Tnn., “sehemu sehemu.”
Tnn., “Huipa chakula miili yote.”