Zaburi 137:1-9

  • Kando ya mito ya Babiloni

    • Nyimbo za Sayuni hazikuimbwa (3, 4)

    • Babiloni kuangamizwa (8)

137  Kando ya mito ya Babiloni,+ hapo ndipo tulipoketi. Tulilia tulipokumbuka Sayuni.+   Juu ya miti ya mierebi iliyo ndani yake,*Tulitundika vinubi vyetu.+   Kwa maana huko, waliotuteka walitaka tuwaimbie,+Waliotudhihaki walitaka tuwatumbuize: “Tuimbieni mojawapo ya nyimbo za Sayuni.”   Tunawezaje kuimba wimbo wa YehovaKatika nchi ya kigeni?   Ikiwa nitakusahau wewe, Ee Yerusalemu,Mkono wangu wa kulia na uwe msahaulifu.*+   Ulimi wangu na ushikamane na kaakaa languNisipokukumbuka,Nisipoliweka Yerusalemu juu yaSababu zangu kuu zaidi za kushangilia.+   Kumbuka, Ee Yehova,Mambo ambayo Waedomu walisema siku ambayo Yerusalemu lilianguka: “Libomoeni! Libomoeni mpaka kwenye misingi yake!”+   Ee binti ya Babiloni, uliye karibu kuangamizwa,+Mwenye furaha ni yule atakayekupa thawabu yakoKwa maovu uliyotutendea.+   Mwenye furaha ni yule atakayewakamata kwa nguvu watoto wakoNa kuwaponda juu ya miamba.+

Maelezo ya Chini

Yaani, Babiloni.
Au labda, “unyauke.”