Zaburi 138:1-8

  • Mungu anajali, ingawa amekwezwa

    • ‘Ulijibu sala yangu’ (3)

    • ‘Hata katikati ya hatari, unaniokoa’ (7)

Wa Daudi. 138  Nitakusifu kwa moyo wangu wote.+ Mbele ya miungu mingine,Nitaimba sifa.*   Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu,*+Nami nitalisifu jina lako+Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako. Kwa maana umelitukuza neno lako na jina lako juu ya vitu vingine vyote.*   Siku niliyokuita, ulinijibu;+Ulinifanya niwe jasiri* na mwenye nguvu.+   Wafalme wote wa dunia watakusifu wewe, Ee Yehova,+Kwa maana watakuwa wamesikia ahadi ulizotoa.   Wataimba kuhusu njia za Yehova,Kwa maana utukufu wa Yehova ni mkuu.+   Ingawa Yehova yuko juu, yeye huwaona wanyenyekevu,+Lakini anajitenga mbali na wenye kiburi.+   Hata nikitembea katikati ya hatari, utanihifadhi hai.+ Unaunyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya maadui wangu;Mkono wako wa kuume utaniokoa.   Yehova atayatimiza mambo yote kwa niaba yangu. Ee Yehova, upendo wako mshikamanifu unadumu milele;+Usiziache kazi za mikono yako.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “Nitaipinga miungu mingine kwa kukupigia muziki.”
Au “mahali pake patakatifu.”
Au labda, “umelitukuza neno lako juu ya jina lako lote.”
Au “niwe na ujasiri katika nafsi yangu.”