Zaburi 139:1-24

  • Mungu anawajua vizuri watumishi wake

    • Huwezi kujificha mbali na roho ya Mungu (7)

    • ‘Nimeumbwa kwa njia inayostaajabisha’ (14)

    • ‘Uliniona nikiwa kiinitete’ (16)

    • “Uniongoze katika njia ya milele” (24)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 139  Ee Yehova, umenichunguza kabisa, nawe unanijua.+   Unajua wakati ninapoketi na wakati ninaposimama.+ Unatambua mawazo yangu kutoka mbali.+   Unanichunguza* ninaposafiri na ninapolala;Unazijua njia zangu zote.+   Kabla sijatamka neno lolote kwa ulimi wangu,Tazama! Ee Yehova, tayari unalijua vizuri.+   Unanizingira nyuma na mbele;Nawe unauweka mkono wako juu yangu.   Ujuzi huo unazidi ufahamu wangu.* Uko juu sana nisiweze kuufikia.*+   Ninaweza kujificha wapi mbali na roho yako,Na ni wapi ninapoweza kukimbia mbali na uso wako?+   Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa huko,Na kama ningetandika kitanda changu Kaburini,* tazama! ungekuwa huko.+   Kama ningeruka kwa mabawa ya mapambazukoIli niishi kando ya bahari iliyo mbali zaidi, 10  Hata huko mkono wako ungeniongozaNa mkono wako wa kuume ungenishika.+ 11  Nikisema: “Hakika giza litanificha!” Basi usiku unaonizunguka utakuwa nuru. 12  Hata giza halitakuwa zito mno kwako,Lakini usiku utakuwa mwangavu kama mchana;+Kwako giza ni sawa na nuru.+ 13  Kwa maana uliziumba figo zangu;Ulinisitiri* katika tumbo la mama yangu.+ 14  Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia inayoogopesha na kustaajabisha.+ Kazi zako zinastaajabisha,+Ninajua* vizuri sana jambo hilo. 15  Mifupa yangu haikufichwa kwakoNilipoumbwa sirini,Nilipofumwa katika sehemu zenye kina za dunia.+ 16  Macho yako hata yaliniona nikiwa kiinitete;Sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chakoKuhusiana na siku ambazo zingeumbwa,Kabla sehemu yoyote haijakuwepo. 17  Kwa hiyo kwangu mimi, mawazo yako ni yenye thamani sana!+ Ee Mungu, jinsi jumla yake ilivyo kubwa sana!+ 18  Nikijaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko chembe za mchanga.+ Nikiamka, bado nipo pamoja nawe.*+ 19  Ee Mungu, laiti ungewaua waovu!+ Ndipo watu wakatili* wangeniondokea, 20  Wale wanaosema mambo mabaya kukuhusu kwa nia ovu;*Wao ni maadui wako wanaolitumia jina lako kwa njia isiyofaa.+ 21  Je, siwachukii wale wanaokuchukia wewe, Ee Yehova,+Na kuwachukia kabisa wale wanaokuasi?+ 22  Ninawachukia kwelikweli;+Hakika wamekuwa maadui wangu. 23  Nichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.+ Nipime, uyajue mawazo yangu yanayonihangaisha.*+ 24  Angalia ikiwa kuna njia yoyote yenye madhara ndani yangu,+Uniongoze+ katika njia ya milele.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Unanipima.”
Au “ni wa ajabu sana kwangu.”
Au “Umezidi kabisa uelewaji wangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au labda, “Ulinifuma pamoja.”
Au “Nafsi yangu inajua.”
Au labda, “nitakuwa bado ninayahesabu.”
Au “wenye hatia ya damu.”
Au “kulingana na mawazo yao.”
Au “yanayonifadhaisha.”