Zaburi 142:1-7

  • Sala ya kuomba aokolewe kutoka kwa watesaji

    • “Sina mahali popote pa kukimbilia” (4)

    • “Ni wewe tu niliye nawe” (5)

Maskili.* Wa Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala. 142  Kwa sauti yangu ninamlilia Yehova anisaidie;+Kwa sauti yangu ninamsihi Yehova anionyeshe kibali.   Ninamwaga mahangaiko yangu mbele zake;Mbele zake ninaeleza taabu yangu+   Roho yangu inapozimia ndani yangu.* Ndipo unapoitazama barabara yangu.+ Katika njia ninayotembea,Wanaficha mtego wa kuninasa.   Tazama upande wa mkono wangu wa kulia uone+Kwamba hakuna yeyote anayenijali.* Sina mahali popote pa kukimbilia;+Hakuna yeyote anayenihangaikia.   Ninakulilia unisaidie, Ee Yehova. Ninasema: “Wewe ni kimbilio langu,+Ni wewe tu niliye nawe* katika nchi ya walio hai.”   Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada,Kwa maana nimeshushwa chini sana. Niokoe kutoka kwa wale wanaonitesa,+Kwa maana wana nguvu kuliko mimi.   Nitoe katika gereza lililo chini ya ardhiIli nilisifu jina lako. Waadilifu na wakusanyike kunizungukaKwa sababu unanitendea kwa fadhili.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “Ninapoishiwa na nguvu.”
Tnn., “anayenitambua.”
Tnn., “Fungu langu.”