Zaburi 142:1-7
Maskili.* Wa Daudi, alipokuwa pangoni.+ Sala.
142 Kwa sauti yangu ninamlilia Yehova anisaidie;+Kwa sauti yangu ninamsihi Yehova anionyeshe kibali.
2 Ninamwaga mahangaiko yangu mbele zake;Mbele zake ninaeleza taabu yangu+
3 Roho yangu inapozimia ndani yangu.*
Ndipo unapoitazama barabara yangu.+
Katika njia ninayotembea,Wanaficha mtego wa kuninasa.
4 Tazama upande wa mkono wangu wa kulia uone+Kwamba hakuna yeyote anayenijali.*
Sina mahali popote pa kukimbilia;+Hakuna yeyote anayenihangaikia.
5 Ninakulilia unisaidie, Ee Yehova.
Ninasema: “Wewe ni kimbilio langu,+Ni wewe tu niliye nawe* katika nchi ya walio hai.”
6 Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada,Kwa maana nimeshushwa chini sana.
Niokoe kutoka kwa wale wanaonitesa,+Kwa maana wana nguvu kuliko mimi.
7 Nitoe katika gereza lililo chini ya ardhiIli nilisifu jina lako.
Waadilifu na wakusanyike kunizungukaKwa sababu unanitendea kwa fadhili.