Zaburi 143:1-12

  • Kiu kwa ajili ya Mungu kama nchi iliyokauka

    • ‘Ninatafakari kazi zako’ (5)

    • “Nifundishe kufanya mapenzi yako” (10)

    • ‘Roho yako nzuri na iniongoze’ (10)

Muziki wa Daudi. 143  Ee Yehova, isikie sala yangu;+Sikiliza sihi yangu ya kuomba msaada. Nijibu katika uaminifu wako na katika uadilifu wako.   Usinihukumu mimi mtumishi wako,Kwa maana hakuna yeyote aliye hai anayeweza kuwa mwadilifu mbele zako.+   Kwa maana adui ananifuatia;Ameuponda uhai wangu ardhini. Amenifanya nikae gizani kama wale waliokufa zamani za kale.   Roho yangu inazimia;*+Moyo wangu umekufa ganzi.+   Ninazikumbuka siku za kale;Ninatafakari utendaji wako wote;+Ninatafakari* kwa bidii kazi ya mikono yako.   Ninakunyooshea mikono yangu;Mimi ni kama nchi iliyokauka yenye kiu kwa ajili yako.+ (Sela)   Nijibu haraka, Ee Yehova;+Nguvu zangu zimefikia* mwisho.+ Usinifiche uso wako,+La sivyo nitakuwa kama wale wanaoshuka shimoni.*+   Acha nisikie upendo wako mshikamanifu asubuhi,Kwa maana ninakutumaini wewe. Nijulishe njia ninayopaswa kutembea ndani yake,+Kwa maana ninakugeukia wewe.*   Niokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Yehova. Ninatafuta ulinzi wako.+ 10  Nifundishe kufanya mapenzi yako,+Kwa maana wewe ni Mungu wangu. Roho yako ni nzuri;Na iniongoze kwenye nchi tambarare.* 11  Ee Yehova, nihifadhi hai kwa ajili ya jina lako. Katika uadilifu wako, niokoe kutoka katika taabu.+ 12  Katika upendo wako mshikamanifu, waangamize* maadui wangu;+Waangamize wote wanaoninyanyasa,+Kwa maana mimi ni mtumishi wako.+

Maelezo ya Chini

Au “Ninaishiwa na nguvu.”
Au “Ninajifunza.”
Au “kaburini.”
Tnn., “Roho yangu imefikia.”
Au “Kwa maana ninakuinulia nafsi yangu.”
Au “katika nchi ya unyoofu.”
Tnn., “wanyamazishe.”