Zaburi 144:1-15

  • Sala ya kuomba ushindi

    • ‘Mwanadamu anayeweza kufa ni nini?’ (3)

    • ‘Maadui na watawanywe’ (6)

    • Watu wa Yehova ni wenye furaha (15)

Wa Daudi. 144  Yehova, Mwamba wangu,+ na asifiwe,Anayeizoeza mikono yangu kwa ajili ya vita,Vidole vyangu kwa ajili ya kupigana.+   Yeye ni upendo wangu mshikamanifu na ngome yangu,Kimbilio langu salama* na mwokozi wangu,Ngao yangu na Yule ambaye nimejificha ndani yake,+Yule anayeyatiisha mataifa chini yangu.+   Ee Yehova, mwanadamu ni nini hata umtambue,Mwana wa mtu anayeweza kufa ni nini hata umkazie uangalifu?+   Mwanadamu ni kama pumzi tu;+Siku zake ni kama kivuli kinachopita.+   Ee Yehova, shusha* mbingu zako uteremke;+Iguse milima na uifanye ifuke moshi.+   Ifanye radi imweke na kuwatawanya maadui;+Piga mishale yako uwavuruge.+   Inyooshe mikono yako kutoka juu;Niokoe na kuninusuru kutoka katika maji mengi,Kutoka katika mkono* wa wageni,+   Ambao kinywa chao kinasema uwongoNa ambao wanainua juu mkono wao wa kulia ili kuapa kwa uwongo.*   Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya.+ Nitakuimbia sifa* kwa kinanda cha nyuzi kumi, 10  Wewe unayewapa wafalme ushindi,*+Wewe unayemwokoa mtumishi wako Daudi kutokana na upanga hatari.+ 11  Niokoe na kuninusuru kutoka katika mkono wa wageni,Ambao vinywa vyao husema uwongoNa ambao wanainua mkono wao wa kulia ili kuapa kwa uwongo. 12  Ndipo wana wetu watakuwa kama mimea michanga inayokua haraka,Mabinti wetu kama nguzo za pembeni zilizochongwa kwa ajili ya jumba la mfalme. 13  Maghala yetu yatafurika mazao ya kila aina;Makundi yetu ya kondoo yataongezeka kwa maelfu, kwa makumi ya maelfu. 14  Ng’ombe wetu, wakiwa na mimba, hawatapatwa na jambo baya* wala mimba kuharibika,Hakutakuwa na kilio cha kuteseka katika viwanja vyetu vya mji. 15  Wenye furaha ni watu wenye hali hizo! Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!+

Maelezo ya Chini

Au “Kilele changu salama.”
Au “kunja.”
Au “udhibiti.”
Tnn., “Na mkono wao wa kulia ni mkono wa kulia wa uwongo.”
Au “Nitakupigia muziki.”
Au “wokovu.”
Au “hawatapasukiwa na mimba.”