Zaburi 145:1-21
Sifa ya Daudi.
א [Aleph]
145 Nitakukweza, Ee Mungu wangu Mfalme,+Nitalisifu jina lako milele na milele.+
ב [Beth]
2 Nitakusifu mchana kutwa;+Nitalisifu jina lako milele na milele.+
ג [Gimel]
3 Yehova ni mkuu na anastahili kabisa kusifiwa;+Ukuu wake hauchunguziki.*+
ד [Daleth]
4 Kizazi baada ya kizazi kitasifu kazi zako;Watasimulia matendo yako yenye nguvu.+
ה [He]
5 Watasema kuhusu fahari tukufu ya ukuu wako+Nami nitatafakari kazi zako zinazostaajabisha.
ו [Waw]
6 Watasema kuhusu matendo yako yanayoogopesha,*Nami nitautangaza ukuu wako.
ז [Zayin]
7 Watabubujikwa na maneno wanapokumbuka wema wako mwingi,+Nao watapaza sauti kwa shangwe kwa sababu ya uadilifu wako.+
ח [Heth]
8 Yehova ni mwenye huruma* na rehema,+Si mwepesi wa hasira, naye ana upendo mwingi mshikamanifu.+
ט [Teth]
9 Yehova ni mwema kwa wote,+Na rehema zake zinaonekana katika kazi zake zote.
י [Yod]
10 Kazi zako zote zitakutukuza, Ee Yehova,+Na washikamanifu wako watakusifu.+
כ [Kaph]
11 Watatangaza utukufu wa ufalme wako+Na kusema kuhusu nguvu zako,+
ל [Lamed]
12 Ili kuwajulisha wanadamu matendo yako yenye nguvu+Na fahari yenye utukufu ya ufalme wako.+
מ [Mem]
13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,Na mamlaka yako hudumu katika vizazi vyote.+
ס [Samekh]
14 Yehova huwategemeza wote wanaoanguka+Na kuwainua juu wote walioinama chini.+
ע [Ayin]
15 Macho yote yanakutazama yakiwa na tumaini;Unawapa chakula chao katika majira yake.+
פ [Pe]
16 Unaufumbua mkono wakoNa kutosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.+
צ [Tsade]
17 Yehova ni mwadilifu katika njia zake zote+Na mshikamanifu katika kila jambo analotenda.+
ק [Qoph]
18 Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia,+Wote wanaomwitia yeye katika ukweli.*+
ר [Resh]
19 Hutosheleza tamaa ya wale wanaomwogopa;+Husikia kilio chao cha kuomba msaada, naye huwaokoa.+
ש [Shin]
20 Yehova huwalinda wale wote wanaompenda,+Lakini atawaangamiza waovu wote.+
ת [Taw]
21 Kinywa changu kitatangaza sifa za Yehova;+Kila kitu kilicho hai na kilisifu* jina lake takatifu milele na milele.+