Zaburi 147:1-20

  • Kuzisifu kazi za Mungu za upendo na zenye nguvu

    • Huwaponya waliovunjika moyo (3)

    • Huziita nyota zote kwa majina (4)

    • Hutoa theluji kama sufu (16)

147  Msifuni Yah!* Ni vema kumwimbia sifa* Mungu wetu;Jinsi inavyopendeza na jinsi inavyofaa sana kumsifu yeye!+   Yehova analijenga Yerusalemu;+Huwakusanya pamoja watu wa Israeli waliotawanywa.+   Huwaponya waliovunjika moyo;Huyafunga majeraha yao.   Huhesabu idadi ya nyota;Zote anaziita kwa majina.+   Bwana wetu ni mkuu naye ana nguvu nyingi;+Uelewaji wake haupimiki.+   Yehova huwainua wapole,+Lakini huwatupa chini waovu.   Mwimbieni Yehova kwa shukrani;Mwimbieni sifa Mungu wetu kwa kinubi,   Yeye anayezifunika mbingu kwa mawingu,Yeye anayeiletea dunia mvua,+Yeye anayechipusha majani+ milimani.   Anawapa wanyama chakula,+Kunguru wachanga wanaokililia.+ 10  Hapendezwi na nguvu za farasi;+Wala havutiwi na miguu yenye nguvu ya mwanamume.+ 11  Yehova anafurahishwa na wale wanaomwogopa,+Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu.+ 12  Mtukuze Yehova, Ee Yerusalemu. Msifu Mungu wako, Ee Sayuni. 13  Huyafanya makomeo ya malango ya jiji lako yawe imara;Huwabariki wana wako walio ndani yako. 14  Huleta amani katika eneo lako;+Hukushibisha kwa ngano bora kabisa.*+ 15  Huituma amri yake duniani;Neno lake hukimbia upesi sana. 16  Hutoa theluji kama sufu;+Hutawanya theluji nyembamba kama majivu tu.+ 17  Huyatupa chini mawe yake ya mvua* kama chembe za mkate.+ Ni nani anayeweza kustahimili baridi yake?+ 18  Hulituma neno lake, nayo inayeyuka. Huufanya upepo wake uvume,+ maji yanatiririka. 19  Anamtangazia Yakobo neno lake,Na Israeli masharti yake na hukumu zake.+ 20  Hajalifanyia hivyo taifa lingine lolote;+Hawajui lolote kuhusu hukumu zake. Msifuni Yah!*+

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “kumpigia muziki.”
Tnn., “mafuta ya ngano.”
Au “Huitupa chini barafu yake.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.