Zaburi 148:1-14

  • Uumbaji wote na umsifu Yehova

    • “Msifuni, enyi malaika wake wote” (2)

    • ‘Msifuni, jua, mwezi, na nyota’ (3)

    • Vijana kwa wazee na wamsifu Mungu (12, 13)

148  Msifuni Yah!* Msifuni Yehova kutoka mbinguni,+Msifuni katika vilele.   Msifuni, enyi malaika wake wote.+ Msifuni, enyi jeshi lake lote.+   Msifuni, enyi jua na mwezi. Msifuni, enyi nyota zote zinazong’aa.+   Msifuni, enyi mbingu zilizo juu kabisa*Na maji yaliyo juu ya mbingu.   Na vilisifu jina la Yehova,Kwa maana aliamuru, navyo vikaumbwa.+   Huvifanya viendelee kuwa imara milele na milele;+Ametoa agizo ambalo halitapitilia mbali.+   Msifuni Yehova kutoka duniani,Enyi viumbe wakubwa wa baharini na pia vilindi vyote vya maji,   Enyi radi na mvua ya mawe, theluji na mawingu mazito,Ewe kimbunga, unayetekeleza neno lake,+   Enyi milima na vilima vyote,+Enyi miti ya matunda na mierezi yote,+ 10  Enyi wanyama wa mwituni+ na wanyama wote wa kufugwa,Enyi viumbe mnaotambaa na ndege wenye mabawa, 11  Enyi wafalme wa dunia, nanyi mataifa yote,Enyi wakuu na waamuzi wote wa dunia,+ 12  Enyi vijana wa kiume na wa kike,*Wazee pamoja na watoto.* 13  Na walisifu jina la Yehova,Kwa maana jina lake peke yake liko juu sana lisiweze kufikiwa.+ Ukuu wake uko juu ya dunia na mbingu.+ 14  Ataikweza nguvu* ya watu wake,Kwa sifa ya washikamanifu wake wote,Ya wana wa Israeli, watu walio karibu naye. Msifuni Yah!*

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Tnn., “mbingu za mbingu.”
Tnn., “mabikira.”
Au “Wakubwa kwa wadogo.”
Tnn., “pembe.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.