Zaburi 149:1-9

  • Wimbo wa kuusifu ushindi wa Mungu

    • Mungu anawafurahia watu wake (4)

    • Heshima ni ya washikamanifu wa Mungu (9)

149  Msifuni Yah!* Mwimbieni Yehova wimbo mpya;+Msifuni katika kutaniko la washikamanifu.+   Watu wa Israeli na washangilie kwa sababu ya Muumba wao Mkuu;+Wana wa Sayuni na washangilie kwa sababu ya Mfalme wao.   Na walisifu jina lake kwa kucheza dansi+Na wamwimbie sifa* kwa tari na kinubi.+   Kwa maana Yehova anawafurahia watu wake.+ Anawapamba wapole kwa wokovu.+   Washikamanifu na washangilie kwa utukufu;Na wapaze sauti kwa shangwe vitandani mwao.+   Nyimbo zinazomsifu Mungu na ziwe kooni mwao,Na upanga wenye makali pande mbili uwe mkononi mwao,   Ili kuyalipiza kisasi mataifaNa kuyaadhibu mataifa,   Ili kuwafunga wafalme wao kwa pinguNa viongozi wao kwa pingu za chuma,   Ili kutekeleza hukumu iliyoandikwa kuwahusu.+ Heshima hii ni ya washikamanifu wake wote. Msifuni Yah!*

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “wampigie muziki.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.