Zaburi 15:1-5

  • Ni nani anayeweza kuwa mgeni katika hema la Yehova?

    • Husema ukweli moyoni mwake (2)

    • Hachongei (3)

    • Hutimiza ahadi hata inapomletea madhara (4)

Muziki wa Daudi. 15  Ee Yehova, ni nani anayeweza kuwa mgeni katika hema lako? Ni nani anayeweza kukaa katika mlima wako mtakatifu?+   Yule anayetembea bila kosa,*+Anayezoea kutenda yaliyo sawa+Na kusema ukweli moyoni mwake.+   Hachongei kwa ulimi wake,+Hamtendei jirani yake jambo lolote ovu,+Naye hawaharibii sifa* rafiki zake.+   Humkataa mtu yeyote anayedharauliwa,+Lakini huwaheshimu wale wanaomwogopa Yehova. Havunji ahadi yake, hata ikimletea hasara.*+   Hakopeshi pesa zake kwa faida,+Naye hakubali rushwa ili kumkandamiza asiye na hatia.+ Yeyote anayefanya mambo hayo hatatikiswa kamwe.*+

Maelezo ya Chini

Au “kwa utimilifu.”
Au “hawaaibishi.”
Tnn., “Havunji kiapo chake, hata kinapomletea hasara.”
Au “hatapepesuka (hatayumbayumba) kamwe.”