Zaburi 15:1-5
Muziki wa Daudi.
15 Ee Yehova, ni nani anayeweza kuwa mgeni katika hema lako?
Ni nani anayeweza kukaa katika mlima wako mtakatifu?+
2 Yule anayetembea bila kosa,*+Anayezoea kutenda yaliyo sawa+Na kusema ukweli moyoni mwake.+
3 Hachongei kwa ulimi wake,+Hamtendei jirani yake jambo lolote ovu,+Naye hawaharibii sifa* rafiki zake.+
4 Humkataa mtu yeyote anayedharauliwa,+Lakini huwaheshimu wale wanaomwogopa Yehova.
Havunji ahadi yake, hata ikimletea hasara.*+
5 Hakopeshi pesa zake kwa faida,+Naye hakubali rushwa ili kumkandamiza asiye na hatia.+
Yeyote anayefanya mambo hayo hatatikiswa kamwe.*+