Zaburi 150:1-6

  • Kila kitu kinachopumua na kimsifu Yah

150  Msifuni Yah!*+ Msifuni Mungu katika mahali pake patakatifu.+ Msifuni katika anga la* nguvu zake.+   Msifuni kwa kazi zake zenye nguvu.+ Msifuni kwa ukuu wake usio na kifani.+   Msifuni kwa kupiga pembe.+ Msifuni kwa kinanda na kinubi.+   Msifuni kwa tari+ na kwa dansi ya mzunguko. Msifuni kwa nyuzi+ na filimbi.*+   Msifuni kwa matoazi yanayolia. Msifuni kwa matoazi yanayogonganishwa.+   Kila kitu kinachopumua—na kimsifu Yah. Msifuni Yah!*+

Maelezo ya Chini

Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au “anga linalotoa ushahidi kuhusu.”
Au “zumari.”
Au “Haleluya!” “Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.