Zaburi 16:1-11

  • Yehova ni Chanzo cha wema

    • “Yehova ni fungu langu” (5)

    • ‘Mawazo yangu hunirekebisha usiku’ (7)

    • ‘Yehova yuko mkono wangu wa kulia’ (8)

    • “Hutaniacha Kaburini” (10)

Miktamu* ya Daudi. 16  Nilinde, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+   Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Yehova, Chanzo changu cha wema.   Na watakatifu walio duniani,Watukufu, ndio ninaopendezwa nao sana.”+   Wale wanaoifuatia miungu mingine huzidisha huzuni yao.+ Sitamimina kamwe matoleo yao ya vinywaji ya damu,Wala midomo yangu haitataja majina yao.+   Yehova ni fungu langu, sehemu niliyogawiwa,+ na kikombe changu.+ Unaulinda urithi wangu.   Nimepimiwa sehemu zinazopendeza. Naam, nimeridhika na urithi wangu.+   Nitamsifu Yehova, ambaye amenipa ushauri.+ Hata wakati wa usiku, mawazo yangu ya ndani kabisa* hunirekebisha.+   Ninamweka Yehova mbele yangu daima.+ Kwa sababu yuko mkono wangu wa kulia, sitatikiswa kamwe.*+   Kwa hiyo moyo wangu unashangilia, nafsi yangu yote ina* shangwe. Nami ninaishi* kwa usalama. 10  Kwa maana hutaniacha* Kaburini.*+ Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.*+ 11  Unanijulisha njia ya uzima.+ Shangwe tele iko mbele zako;*+Kuna furaha* kwenye mkono wako wa kuume milele.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”
Au “sitapepesuka (sitayumbayumba) kamwe.”
Tnn., “utukufu wangu una.”
Au “Mwili wangu huishi.”
Au “hutaiacha nafsi yangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au labda, “aone uharibifu.”
Tnn., “pamoja na uso wako.”
Au “uzuri.”