Zaburi 17:1-15

  • Sala ya kuomba ulinzi

    • “Umeuchunguza moyo wangu” (3)

    • “Katika kivuli cha mabawa yako” (8)

Sala ya Daudi. 17  Sikia sihi yangu ya kuomba haki, Ee Yehova;Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada;Sikiliza sala yangu ninayosema bila udanganyifu.+   Nawe ufanye uamuzi wa haki kwa niaba yangu;+Macho yako na yaone yaliyo sawa.   Umeuchunguza moyo wangu, umenikagua wakati wa usiku;+Umenisafisha;+Utagundua kwamba sijapanga njama ya kutenda uovu wowote,Na kinywa changu hakijatenda dhambi.   Kuhusiana na shughuli za wanadamu,Kulingana na neno la midomo yako, ninaepuka njia za mnyang’anyi.+   Acha hatua zangu zibaki kwenye njia zakoIli miguu yangu isijikwae.+   Ninakuita wewe, kwa sababu utanijibu,+ Ee Mungu. Nitegee sikio lako.* Sikia maneno yangu.+   Onyesha upendo wako mshikamanifu kwa njia yenye kustaajabisha,+Ee Mwokozi wa wale wanaokimbilia mkono wako wa kuumeKutoka kwa wale wanaokuasi.   Nilinde kama mboni ya jicho lako;+Nifiche katika kivuli cha mabawa yako.+   Nilinde kutokana na waovu wanaonishambulia,Kutokana na maadui wangu* wanaoweza kufa ambao wananizingira.+ 10  Wamekufa ganzi;*Kwa kinywa chao wanaongea kwa kiburi; 11  Sasa wanatuzingira;+Wanatafuta nafasi ya kutuangusha.* 12  Yeye ni kama simba anayetamani kurarua windo lake vipandevipande,Kama mwanasimba anayenyemelea mafichoni. 13  Inuka, Ee Yehova, ukabiliane naye+ na kumwangusha chini;Niokoe* kutoka kwa mwovu kwa kutumia upanga wako; 14  Niokoe kwa mkono wako, Ee Yehova,Kutoka kwa watu wa ulimwengu huu,* ambao fungu lao liko katika maisha haya,+Wale ambao unawajaza kwa vitu vizuri unavyoandaa+Na ambao huwaachia urithi wana wao wengi. 15  Lakini mimi, nitauona uso wako kwa sababu ya uadilifu wangu;Ninaridhika kuamka mbele zako.*+

Maelezo ya Chini

Au “Inama chini na unisikilize.”
Au “maadui wangu walio dhidi ya nafsi.”
Au “Wamefunikwa na mafuta yao wenyewe.”
Au “kututupa chini.”
Au “Iokoe nafsi yangu.”
Au “mfumo huu wa mambo.”
Au “kuona sura yako.”