Zaburi 2:1-12

  • Yehova na mtiwa-mafuta wake

    • Yehova anayacheka mataifa (4)

    • Yehova amweka mfalme wake (6)

    • Mheshimuni mwana (12)

2  Kwa nini mataifa yana msukosukoNa watu wananong’ona* kuhusu jambo lisilo na maana?+   Wafalme wa dunia wanajipangaNa maofisa wakuu wanakusanyika* pamoja kama kitu kimoja+Dhidi ya Yehova na dhidi ya mtiwa-mafuta* wake.+   Wanasema: “Na tuzikate pingu zaoNa kuzitupa kamba zao!”   Yule anayeketi kwenye kiti cha ufalme mbinguni atacheka;Yehova atawadhihaki.   Wakati huo ataongea nao kwa hasira yakeNa kuwatisha kwa hasira yake inayowaka,   Akisema: “Mimi mwenyewe nimemweka mfalme wangu+Juu ya Sayuni,+ mlima wangu mtakatifu.”   Acheni nitangaze agizo la Yehova;Aliniambia: “Wewe ni mwanangu;+Leo nimekuwa baba yako.+   Niombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wakoNa miisho ya dunia kuwa miliki yako.+   Utawavunja kwa fimbo ya mfalme ya chuma,+Nawe utawavunjavunja kama chombo cha udongo.”+ 10  Basi sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu;Kubalini kurekebishwa,* enyi waamuzi wa dunia. 11  Mtumikieni Yehova kwa woga,Na mshangilie mkitetemeka. 12  Mheshimuni* mwana,+ la sivyo Mungu atawaka hasiraNanyi mtaangamia kutoka njiani,+Kwa maana hasira Yake huwaka upesi. Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia Yeye.

Maelezo ya Chini

Au “wanatafakari kuhusu.”
Au “wanashauriana.”
Au “Kristo.”
Au “onyo.”
Tnn., “Mbusuni.”