Zaburi 20:1-9

  • Wokovu kwa ajili ya mfalme mtiwa-mafuta wa Mungu

    • Wengine hutegemea magari ya vita na farasi, “lakini sisi tunaliitia jina la Yehova” (7)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 20  Yehova na akujibu katika siku ya taabu. Jina la Mungu wa Yakobo na likulinde.+   Na akuletee msaada kutoka mahali patakatifu+Na kukutegemeza kutoka Sayuni.+   Na akumbuke matoleo yako yote ya zawadi;Na aikubali kwa upendeleo* dhabihu yako ya kuteketezwa. (Sela)   Na atosheleze tamaa za moyo wako+Na kufanikisha mipango yako yote.*   Tutapaza sauti kwa shangwe kwa sababu ya matendo yako ya wokovu;+Tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+ Yehova na atimize maombi yako yote.   Sasa ninajua kwamba Yehova humwokoa mtiwa-mafuta wake.+ Humjibu kutoka katika mbingu zake takatifuKwa wokovu* mkubwa kupitia mkono wake wa kuume.+   Wengine hutegemea magari ya vita na wengine farasi,+Lakini sisi tunaliitia jina la Yehova Mungu wetu.+   Wamedondoka na kuanguka,Lakini sisi tumeinuka na kurudishwa.+   Ee Yehova, mwokoe mfalme!+ Atatujibu siku ambayo tutaomba msaada.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “aione kuwa mafuta.”
Au “ushauri wako wote.”
Au “ushindi.”