Zaburi 21:1-13

  • Baraka kwa mfalme anayemtumaini Yehova

    • Mfalme apewa maisha marefu (4)

    • Maadui wa Mungu watashindwa (8-12)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 21  Ee Yehova, mfalme hushangilia kwa sababu ya nguvu zako;+Jinsi anavyoshangilia sana kwa sababu ya matendo yako ya wokovu!+   Umetosheleza tamaa ya moyo wake,+Nawe hujamnyima ombi la midomo yake. (Sela)   Kwa maana unamlaki kwa baraka tele;Unamvika taji la dhahabu bora* kichwani.+   Alikuomba uhai, nawe ukampa,+Maisha marefu,* milele na milele.   Matendo yako ya wokovu humletea utukufu mkubwa.+ Unamtunukia adhama na fahari.   Unamfanya awe na baraka milele;+Unamfanya afurahi kwa shangwe ya kuwa mbele zako.*+   Kwa maana mfalme anamtumaini Yehova;+Kwa sababu ya upendo mshikamanifu wa Aliye Juu Zaidi, hatatikiswa kamwe.*+   Mkono wako utawapata maadui wako wote;Mkono wako wa kuume utawapata wale wanaokuchukia.   Utawafanya wawe kama tanuru lenye moto mkali utakapofika wakati ulioweka wa kuwakazia uangalifu. Yehova atawameza kwa hasira yake, na moto utawateketeza kabisa.+ 10  Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani,Na uzao wao kutoka kati ya wanadamu. 11  Kwa maana walikusudia kukutendea maovu;+Wamepanga njama ambazo hazitafanikiwa.+ 12  Kwa maana utawafanya wakimbie+Kwa kuwalenga* kwa upinde wako.* 13  Inuka, Ee Yehova, katika nguvu zako. Tutauimbia sifa* uwezo wako.

Maelezo ya Chini

Au “iliyosafishwa.”
Tnn., “Urefu wa siku.”
Tnn., “mbele za uso wako.”
Au “hatapepesuka (hatayumbayumba) kamwe.”
Tnn., “kulenga nyuso zao.”
Tnn., “kamba zako za upinde.”
Tnn., “Tutauimbia na kuupigia muziki.”