Zaburi 22:1-31

  • Baada ya kukata tamaa, amsifu Mungu

    • “Mungu wangu, kwa nini umeniacha?” (1)

    • “Wanalipigia kura vazi langu” (18)

    • Kumsifu Mungu kutanikoni (22, 25)

    • Dunia yote itamwabudu Mungu (27)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Paa Jike wa Mapambazuko.”* Muziki wa Daudi. 22  Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?+ Kwa nini uko mbali usiweze kuniokoa,Mbali na vilio vyangu vya maumivu makali?+   Mungu wangu, ninaendelea kukuita wakati wa mchana, nawe hunijibu;+Na wakati wa usiku sinyamazi.   Lakini wewe ni mtakatifu,+Umezungukwa na* sifa za Israeli.   Baba zetu walikutumaini wewe;+Walikutumaini, nawe ulikuwa ukiwaokoa.+   Walikulilia kwa sauti, wakaokolewa;Walikutumaini, nao hawakukatishwa tamaa.*+   Lakini mimi ni mnyoo wala si mwanadamu,Ninadhihakiwa na wanadamu na kudharauliwa na watu.*+   Wote wanaoniona hunikejeli;+Wanafyonya midomo na kutikisa vichwa vyao kwa dharau:+   “Alijikabidhi mwenyewe kwa Yehova. Acha Yeye amwokoe! Acha Yeye amwokoe, kwa sababu Yeye anampenda sana!”+   Wewe ndiye uliyenitoa tumboni,+Ni Wewe uliyenifanya nihisi nikiwa salama kwenye matiti ya mama yangu. 10  Nimewekwa chini ya utunzaji wako* tangu nilipozaliwa;Tangu nilipokuwa katika tumbo la mama yangu, umekuwa Mungu wangu. 11  Usikae mbali nami, kwa maana taabu iko karibu+Nami sina msaidizi mwingine.+ 12  Ng’ombe dume wengi wachanga wananizunguka;+Ng’ombe dume wenye nguvu wa Bashani wananizingira.+ 13  Wanafungua vinywa vyao wazi dhidi yangu,+Kama simba anayenguruma ambaye anararua windo lake vipandevipande.+ 14  Nimemwagwa kama maji;Mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu umekuwa kama nta;+Unayeyuka katika sehemu zangu za ndani kabisa.+ 15  Nguvu zangu zimekauka kama kigae;+Ulimi wangu unashikamana na fizi zangu;+Unanishusha chini kwenye mavumbi ya kifo.+ 16  Kwa maana mbwa wananizunguka;+Wananizingira kama kundi la watenda maovu,+Kama simba, wanaishambulia mikono yangu na miguu yangu.+ 17  Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote.+ Wananitazama na kunikodolea macho. 18  Wanagawana mavazi yangu,Nao wanalipigia kura vazi langu.+ 19  Lakini wewe, Ee Yehova, usiendelee kukaa mbali.+ Wewe ni nguvu zangu; njoo haraka unisaidie.+ 20  Niokoe* kutoka kwa upanga,Uhai wangu wenye thamani* kutoka katika makucha ya* mbwa;+ 21  Niokoe kutoka katika kinywa cha simba+ na pembe za ng’ombe dume wa mwituni;Nijibu na uniokoe. 22  Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu;+Katikati ya kutaniko nitakusifu.+ 23  Ninyi mnaomwogopa Yehova, msifuni! Enyi nyote uzao wa* Yakobo, mtukuzeni!+ Mwogopeni yeye, enyi nyote uzao wa* Israeli. 24  Kwa maana hajadharau wala kuchukizwa na mateso ya yule anayekandamizwa;+Hajauficha uso wake kutoka kwake.+ Alipomlilia amsaidie, alisikia.+ 25  Nitakusifu katika kutaniko kubwa;+Nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanaomwogopa. 26  Wapole watakula na kushiba;+Wale wanaomtafuta Yehova watamsifu.+ Na ufurahie maisha* milele. 27  Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Yehova. Familia zote za mataifa zitainama chini mbele zako.+ 28  Kwa maana ufalme ni wa Yehova;+Anayatawala mataifa. 29  Watu wote wenye ufanisi* duniani watakula na kumwinamia;Wote wanaoshuka mavumbini watapiga magoti mbele zake;Hakuna yeyote kati yao anayeweza kuokoa uhai wao.* 30  Wazao wao watamtumikia;*Kizazi kitakachokuja kitaambiwa kumhusu Yehova. 31  Watakuja na kusimulia uadilifu wake. Watawaambia watu ambao bado hawajazaliwa mambo aliyofanya.

Maelezo ya Chini

Labda ni sauti au mtindo wa muziki.
Au “Umeketi kwenye kiti cha ufalme kati ya (juu ya).”
Au “hawakuaibishwa.”
Au “Mimi ni fedheha kwa wanadamu na ninadharauliwa na watu.”
Tnn., “Nimetupwa kwako.”
Au “Iokoe nafsi yangu.”
Tnn., “Uhai pekee nilio nao,” yaani, nafsi yake.
Tnn., “mkono wa.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “Moyo wako na uishi.”
Tnn., “wanene.”
Au “nafsi zao.”
Tnn., “Mbegu itamtumikia.”