Zaburi 23:1-6

  • “Yehova ni Mchungaji wangu”

    • “Sitakosa chochote” (1)

    • “Huniburudisha” (3)

    • “Kikombe changu kimejazwa vizuri” (5)

Muziki wa Daudi. 23  Yehova ni Mchungaji wangu.+ Sitakosa chochote.+   Hunilaza katika malisho yenye majani mengi;Huniongoza kwenye sehemu za kupumzika zenye maji mengi.*+   Huniburudisha.*+ Huniongoza katika njia za* uadilifu kwa ajili ya jina lake.+   Hata nikitembea katika bonde lenye kivuli kizito,+Siogopi madhara yoyote,+Kwa maana wewe uko pamoja nami;+Fimbo yako na gongo lako hunipa uhakika.*   Wewe huniandalia meza mbele ya maadui wangu.+ Unakiburudisha* kichwa changu kwa mafuta;+Kikombe changu kimejazwa vizuri.+   Kwa hakika wema na upendo mshikamanifu utanifuatia sikuzote za maisha yangu,+Nami nitakaa katika nyumba ya Yehova siku zangu zote.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “maji matulivu.”
Au “Huiburudisha nafsi yangu.”
Tnn., “mapito ya; vijia vya.”
Au “hunifariji.”
Au “Unakipaka.”