Zaburi 24:1-10

  • Mfalme mtukufu aingia malangoni

    • ‘Dunia ni ya Yehova’ (1)

Muziki wa Daudi. 24  Dunia na vyote vilivyomo ni vya Yehova,+Nchi inayozaa na wale wanaokaa ndani yake.   Kwa maana ameiweka imara kabisa juu ya bahari+Na kuiweka imara kabisa juu ya mito.   Ni nani anayeweza kuupanda mlima wa Yehova,+Na ni nani anayeweza kusimama mahali pake patakatifu?   Yeyote mwenye mikono isiyo na hatia na mwenye moyo safi,+Ambaye hajaapa kwa uwongo kwa uhai Wangu,*Wala kuapa kwa udanganyifu.+   Atapokea baraka kutoka kwa Yehova+Na uadilifu* kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.+   Hiki ndicho kizazi cha wale wanaomtafuta,Cha wale wanaoutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)   Inueni vichwa vyenu, enyi malango;+Fungukeni,* enyi milango ya kale,Ili Mfalme mtukufu aingie!+   Mfalme huyu mtukufu ni nani? Yehova, mwenye nguvu na hodari,+Yehova, hodari katika vita.+   Inueni vichwa vyenu, enyi malango;+Fungukeni, enyi milango ya kale,Ili Mfalme mtukufu aingie! 10  Mfalme huyu mtukufu ni nani? Yehova wa majeshi—yeye ndiye Mfalme mtukufu.+ (Sela)

Maelezo ya Chini

Au “nafsi Yangu,” ikirejelea mtu kuapa kwa uhai wa Yehova.
Au “haki.”
Au “Inukeni.”