Zaburi 25:1-22

  • Sala ya kuomba mwongozo na msamaha

    • “Nifundishe vijia vyako” (4)

    • “Urafiki wa karibu pamoja na Yehova” (14)

    • “Unisamehe dhambi zangu zote” (18)

Wa Daudi. א [Aleph] 25  Nakugeukia wewe,* Ee Yehova. ב [Beth]   Mungu wangu, ninakutumaini wewe;+Usiruhusu niaibishwe.+ Usiruhusu maadui wangu wanicheke.+ ג [Gimel]   Kwa hakika hakuna yeyote anayekutumaini atakayeaibishwa,+Lakini aibu inawangoja wale wanaotenda kwa hila bila sababu.+ ד [Daleth]   Nijulishe njia zako, Ee Yehova;+Nifundishe vijia vyako.+ ה [He]   Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha,+Kwa maana wewe ni Mungu wa wokovu wangu. ו [Waw] Ninakutumaini mchana kutwa. ז [Zayin]   Kumbuka rehema zako, Ee Yehova, na upendo wako mshikamanifu,+Ambazo umedhihirisha sikuzote.*+ ח [Heth]   Usikumbuke dhambi na makosa niliyotenda nilipokuwa kijana. Nikumbuke kulingana na upendo wako mshikamanifu,+Kwa ajili ya wema wako, Ee Yehova.+ ט [Teth]   Yehova ni mwema na mnyoofu.+ Ndiyo sababu yeye huwafundisha watenda dhambi njia wanayopaswa kuishi.+ י [Yod]   Atawaongoza wapole katika yaliyo sawa,*+Naye atawafundisha wapole njia yake.+ כ [Kaph] 10  Njia zote za Yehova ni upendo mshikamanifu na uaminifuKwa wale wanaoshika agano lake+ na vikumbusho vyake.+ ל [Lamed] 11  Kwa ajili ya jina lako, Ee Yehova,+Nisamehe kosa langu, ingawa ni kubwa. מ [Mem] 12  Ni nani anayemwogopa Yehova?+ Atamfundisha kuhusu njia anayopaswa kuchagua.+ נ [Nun] 13  Atajionea* yaliyo mema,+Na wazao wake wataimiliki* dunia.+ ס [Samekh] 14  Urafiki wa karibu pamoja na Yehova ni wa wale wanaomwogopa,+Naye huwajulisha agano lake.+ ע [Ayin] 15  Macho yangu humtazama Yehova daima,+Kwa maana ataiweka huru miguu yangu kutoka katika wavu.+ פ [Pe] 16  Nielekezee uso wako na kunionyesha kibali,Kwa maana niko peke yangu na sina uwezo. צ [Tsade] 17  Taabu za moyo wangu zimeongezeka;+Niondolee maumivu yangu makali. ר [Resh] 18  Yaone mateso yangu na shida yangu,+Nawe unisamehe dhambi zangu zote.+ 19  Tazama jinsi maadui wangu walivyo wengiNa jinsi wanavyonichukia vikali. ש [Shin] 20  Ulinde uhai wangu* na uniokoe.+ Usiruhusu niaibishwe, kwa maana nimekukimbilia wewe. ת [Taw] 21  Utimilifu na unyoofu na vinilinde,+Kwa maana ninakutumaini wewe.+ 22  Ee Mungu, mwokoe* Israeli kutoka katika taabu zake zote.

Maelezo ya Chini

Au “Nainua nafsi yangu kwako.”
Au “Ambazo ni za tangu nyakati za kale.”
Tnn., “katika hukumu.”
Au “Nafsi yake itajionea.”
Tnn., “mbegu yake itamiliki.”
Au “Ilinde nafsi yangu.”
Tnn., “mkomboe.”