Zaburi 26:1-12

  • Kutembea katika utimilifu

    • “Nichunguze, Ee Yehova” (2)

    • Kuepuka marafiki wabaya (4, 5)

    • ‘Nitapiga mwendo kuzunguka madhabahu ya Mungu’ (6)

Wa Daudi. 26  Unihukumu, Ee Yehova, kwa maana nimetembea katika utimilifu wangu;+Nimemtumaini Yehova bila kuyumbayumba.+   Nichunguze, Ee Yehova, na unijaribu;Safisha mawazo yangu ya ndani kabisa* na pia moyo wangu.+   Kwa maana upendo wako mshikamanifu uko mbele yangu daima,Nami ninatembea katika kweli yako.+   Sishirikiani* na watu wadanganyifu,+Nami huwaepuka wale wanaoficha jinsi walivyo.*   Ninachukia kundi la waovu,+Nami ninakataa kushirikiana* na waovu.+   Nitanawa mikono yangu katika ukosefu wa hatia,Nami nitapiga mwendo kuzunguka madhabahu yako, Ee Yehova,   Ili niifanye sauti ya utoaji shukrani isikike+Na kutangaza kazi zako zote zinazostaajabisha.   Yehova, ninaipenda nyumba ambamo unakaa,+Mahali ambapo utukufu wako hukaa.+   Usinifagilie mbali* pamoja na watenda dhambi+Wala kuniua pamoja na watu wakatili,* 10  Ambao mikono yao hutenda matendo ya* aibu,Na ambao mkono wao wa kulia umejaa rushwa. 11  Lakini mimi, nitatembea katika utimilifu wangu. Niokoe* na kunionyesha kibali. 12  Mguu wangu umesimama mahali tambarare;+Katika kutaniko kubwa,* nitamsifu Yehova.+

Maelezo ya Chini

Au “hisia zangu za ndani kabisa.” Tnn., “figo zangu.”
Tnn., “Siketi.”
Au “sichangamani na wanafiki.”
Tnn., “kuketi.”
Tnn., “Usiifagilie mbali nafsi yangu.”
Au “watu wanaomwaga damu.”
Au “mwenendo wa.”
Tnn., “Nikomboe.”
Tnn., “makusanyiko.”