Zaburi 27:1-14

  • Yehova ni ngome ya uhai wangu

    • Kulithamini hekalu la Mungu (4)

    • Yehova anajali hata ikiwa wazazi hawajali (10)

    • “Mtumaini Yehova” (14)

Wa Daudi. 27  Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu. Nimwogope nani?+ Yehova ni ngome ya uhai wangu.+ Nimhofu nani?   Waovu waliponishambulia ili waunyafue mwili wangu,+Wapinzani wangu na maadui wangu ndio waliojikwaa na kuanguka.   Hata jeshi likipiga kambi ili kunishambulia,Moyo wangu hautaogopa.+ Hata vita vikizuka dhidi yangu,Bado nitaendelea kuwa jasiri.   Nimemwomba Yehova jambo moja—Ndilo nitakalolitafuta—Kwamba nikae katika nyumba ya Yehova sikuzote za maisha yangu,+Ili kuutazama uzuri wa YehovaNa kutazama kwa uthamini* hekalu lake.*+   Kwa maana atanificha katika banda lake siku ya msiba;+Atanificha mahali pa siri katika hema lake;+Ataniweka juu kwenye mwamba.+   Sasa kichwa changu kiko juu sana ya maadui wangu wanaonizingira;Nitatoa dhabihu katika hema lake kwa kelele za shangwe;Nitamwimbia sifa* Yehova.   Nisikie, Ee Yehova, ninapolia kwa sauti;+Nionyeshe kibali na kunijibu.+   Moyo wangu umesema hivi kwa niaba yako: “Utafute uso wangu.” Nitautafuta uso wako, Ee Yehova.+   Usinifiche uso wako.+ Usimfukuze kwa hasira mtumishi wako. Wewe ni msaidizi wangu;+Usinitupe wala usiniache, Mungu wa wokovu wangu. 10  Hata baba yangu na mama yangu wakiniacha,+Yehova mwenyewe atanichukua.+ 11  Nifundishe njia yako, Ee Yehova,+Niongoze katika kijia cha unyoofu kwa sababu ya maadui wangu. 12  Usinitie mikononi mwa maadui wangu,+Kwa maana mashahidi wa uwongo wameinuka dhidi yangu,+Nao wanatoa vitisho vya kunitendea kwa ukatili. 13  Ningekuwa wapi ikiwa singekuwa na imaniKwamba nitauona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai?*+ 14  Mtumaini Yehova;+Uwe jasiri na uwe na moyo mkuu.+ Naam, mtumaini Yehova.

Maelezo ya Chini

Au “kutazama kwa kutafakari.”
Au “mahali pake patakatifu.”
Au “Nitampigia muziki.”
Au labda, “Kwa hakika nina imani kwamba nitauona wema wa Yehova katika nchi ya walio hai.”