Zaburi 28:1-9

  • Sala ya mtunga zaburi yasikiwa

    • ‘Yehova ni nguvu zangu na ngao yangu’ (7)

Wa Daudi. 28  Ninaendelea kukulilia wewe, Ee Yehova Mwamba wangu;+Usiwe kama kiziwi kwangu. Ukininyamazia,Nitakuwa kama wale wanaoshuka shimoni.*+   Sikia sihi zangu ninapokulilia unisaidieNinapoinua mikono yangu kuelekea chumba cha ndani zaidi cha mahali pako patakatifu.+   Usinikokote pamoja na waovu, pamoja na wale wanaotenda mambo yanayodhuru,+Wale wanaoongea na jirani yao maneno ya amani lakini uovu uko mioyoni mwao.+   Walipe kulingana na matendo yao,+Kulingana na mazoea yao maovu. Walipe kulingana na kazi ya mikono yao,Kulingana na mambo waliyotenda.+   Kwa maana hawazingatii utendaji wa Yehova,+Wala kazi ya mikono yake.+ Atawabomoa kabisa naye hatawajenga.   Yehova na asifiwe,Kwa maana amesikia sihi zangu za kuomba msaada.   Yehova ni nguvu zangu+ na ngao yangu;+Moyo wangu unamtumaini yeye.+ Amenisaidia, na moyo wangu unashangilia,Kwa hiyo nitamsifu kwa wimbo wangu.   Yehova ni nguvu kwa watu wake;Yeye ni ngome, anamletea mtiwa-mafuta wake wokovu mkubwa.+   Waokoe watu wako, na uubariki urithi wako.+ Wachunge na kuwabeba mikononi mwako milele.+

Maelezo ya Chini

Au “kaburini.”