Zaburi 29:1-11

  • Sauti ya Yehova yenye nguvu

    • Abuduni katika mapambo matakatifu (2)

    • “Mungu mtukufu hunguruma” (3)

    • Yehova huwapa nguvu watu wake (11)

Muziki wa Daudi. 29  Mpeni Yehova anachostahili, enyi wana wa watu hodari,Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+   Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili. Mwinamieni* Yehova katika mapambo matakatifu.*   Sauti ya Yehova husikika juu ya maji;Mungu mtukufu hunguruma.+ Yehova yuko juu ya maji mengi.+   Sauti ya Yehova ina nguvu;+Sauti ya Yehova ina fahari.   Sauti ya Yehova inavunja mierezi;Naam, Yehova anaipasua-pasua mierezi ya Lebanoni.+   Hufanya Lebanoni* irukeruke kama ndama,Na Sirioni+ kama ng’ombe dume mchanga wa mwituni.   Sauti ya Yehova hupiga kwa miali ya moto;+   Sauti ya Yehova huifanya nyika itetemeke;+Yehova huifanya nyika ya Kadeshi+ itetemeke.   Sauti ya Yehova humfanya paa atetemeke na kuzaaNayo huivua kabisa misitu.+ Na wote walio katika hekalu lake husema: “Utukufu!” 10  Yehova huketi kwenye kiti cha ufalme juu ya mafuriko ya maji;*+Yehova huketi kwenye kiti cha ufalme akiwa Mfalme milele.+ 11  Yehova atawapa nguvu watu wake.+ Yehova atawabariki watu wake kwa amani.+

Maelezo ya Chini

Au “Mwabuduni.”
Au labda, “kwa sababu ya fahari ya utakatifu wake.”
Inaonekana ni safu ya milima ya Lebanoni.
Au “bahari ya mbinguni.”