Zaburi 3:1-8

  • Kumtumaini Mungu licha ya hatari

    • ‘Kwa nini maadui wamekuwa wengi sana?’ (1)

    • “Wokovu ni wa Yehova” (8)

Muziki wa Daudi alipokuwa akimkimbia Absalomu mwanawe.+ 3  Ee Yehova, kwa nini maadui wangu wamekuwa wengi sana?+ Kwa nini watu wengi sana wanainuka dhidi yangu?+   Wengi wanasema hivi kunihusu:* “Mungu hatamwokoa.”+ (Sela)*   Lakini wewe, Ee Yehova, ni ngao kunizunguka,+Utukufu wangu+ na Yule anayekiinua kichwa changu.+   Nitamlilia Yehova kwa sauti kubwa,Naye atanijibu kutoka kwenye mlima wake mtakatifu.+ (Sela)   Nitajilaza chini na kulala usingizi;Nami nitaamka nikiwa salama,Kwa maana Yehova anaendelea kunitegemeza.+   Siogopi makumi ya maelfuWaliojipanga dhidi yangu kila upande.+   Inuka, Ee Yehova! Niokoe,+ Ee Mungu wangu! Kwa maana utawapiga maadui wangu wote kwenye utaya;Utayavunja meno ya waovu.+   Wokovu ni wa Yehova.+ Baraka yako iko juu ya watu wako. (Sela)

Maelezo ya Chini

Au “kuihusu nafsi yangu.”
Angalia Kamusi.