Zaburi 30:1-12

  • Maombolezo yabadilishwa kuwa shangwe

    • Kibali cha Mungu hudumu maisha yote (5)

Muziki. Wimbo wa kuizindua nyumba. Wa Daudi. 30  Nitakukweza, Ee Yehova, kwa maana umeniinua* juu;Hukuruhusu maadui wangu washangilie juu yangu.+   Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+   Ee Yehova, umeniinua* kutoka Kaburini.*+ Ulifanya niendelee kuwa hai; uliniokoa nisizame shimoni.*+   Mwimbieni sifa* Yehova, enyi washikamanifu wake,+Lishukuruni jina lake takatifu;*+   Kwa sababu hasira yake ni ya muda mfupi tu,+Lakini kibali chake* hudumu maisha yote.+ Huenda kukawa na kilio jioni, lakini asubuhi, kuna kilio cha shangwe.+   Nilipokuwa na amani, nilisema: “Sitatikiswa kamwe.”*   Ee Yehova, nilipokuwa na kibali chako,* ulinifanya niwe imara kama mlima.+ Lakini ulipouficha uso wako, niliogopa.+   Niliendelea kukulilia wewe, Ee Yehova;+Nami niliendelea kukusihi wewe, Ee Yehova, unionyeshe kibali.   Kuna faida gani nikifa,* nikishuka shimoni?*+ Je, mavumbi yatakusifu?+ Je, yatasimulia kuhusu uaminifu wako?+ 10  Sikia, Ee Yehova, na unionyeshe kibali.+ Ee Yehova, uwe msaidizi wangu.+ 11  Umebadili maombolezo yangu kuwa dansi;Umenivua nguo zangu za magunia, nawe unanivisha shangwe, 12  Ili niimbe* sifa yako, nisinyamaze. Ee Yehova Mungu wangu, nitakusifu milele.

Maelezo ya Chini

Au “umenivuta.”
Au “umeiinua nafsi yangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “kaburini.”
Au “Mpigieni muziki.”
Tnn., “Ushukuruni ukumbusho wake.”
Au “nia yake njema.”
Au “Sitapepesuka (sitayumbayumba) kamwe.”
Au “nia yako njema.”
Tnn., “Damu yangu ina faida gani.”
Au “kaburini.”
Au “Ili utukufu wangu uimbe.”